Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Spika, umiliki wa vitalu vya uwindaji, tamko la Serikali la tarehe 23 Januari, 2017 kuwafutia wamiliki wa vitalu vya kuwindia biashara kutoka miaka mitano hadi miwili kumesababisha biashara hii kuyumba. Biashara ya utalii wa uwindaji huwa inaandaliwa kwa muda mrefu sana na uwekezaji wake ni wa gharama ya juu inayohusu kukarabati miundombinu mbalimbali. Aina hii ya utalii ni ya bei ya juu, sasa ni karibia dola 60,000 mpaka dola 80,000 kwa mtalii kuja kwenye utalii huu. Hivyo watalii wanataka wawe na uhakika wa deposit zao watakazotoa. Pamekuwa hakuna utulivu tena katika tasnia hii. Wawekezaji hawana uhakika na biashara zao hadi kupelekea wengine kuvirudisha vitalu hivyo.

Mheshimiwa Spika, ushauri, kama Serikali inataka kuuza kwa mnada hivyo vitalu kwa nini visiuzwe na vile vilivyo wazi kama jaribio kulikoni kuvuruga wawekezaji ambao tayari wameshatumia fedha nyingi kuendeleza vitalu vyao?

Mheshimiwa Spika, sekta ya utalii inachangia katika pato la Taifa asilimia 17.5 na inaweza kuchangia vizuri zaidi kama tukiweza kuendeleza Southern Circuit, utalii wa utamaduni na michezo kwa mfano Kilimanjaro International Marathon inakuwa ni kivutio kikubwa sana mbali na riadha, watu wakimaliza kukimbia huenda kupanda Mlima Kilimanjaro na kutembelea mbuga zetu lakini wengi wanarudi zaidi ya mara moja. Lakini safari ya kwenda Selous lakini tour ya kwenda huko ni ghali sana, hakuna hoteli za kutosha na zilizopo ni za ghali sana.

Mheshimiwa Spika, katika sekta hii kumekuwepo na tozo nyingi sana takribani tozo 36 tofauti. Wafanyabiashara hawakatai kulipa kodi lakini kwa nini zisiunganishwe zikalipwa sehemu moja ili kuondoa usumbufu hata dakika moja tu ya mfanyabiashara ni fedha. Unakuta ofisi ya mtu (tours operation) imezungukwa na leseni nyingi kama mapambo.

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa hivi bado Serikali haijaelekeza ipasavyo katika utalii wa picha, mfano kuna baadhi ya watalii wanataka wafanye utalii wa kupiga picha wakati wakipanda mlima, lakini huu ukiritimba uliopo mpaka apate kibali cha kupiga picha ni shughuli, havitoki kwa wakati mpaka mtalii huwa ana-concel safari yake.

Mheshimiwa Spika, Mlima Kilimanjaro; Serikali kwa kushirikiana na nchi ya Ujerumani walikuwa waweke clinical toilet katika njia za kupanda Mlima Machame, Umbwe route, Lemosho, Landorosi lakini mpaka leo Serikali haijaweza kuviweka vyoo hivyo. Je, ule mchakato umeishia wapi? Hii inasaidia sana kutunza mazingira (usafi) sababu kule crater kunatia aibu ni kuchafu sana.

Suala lingine mara nyingi nimekuwa nikishauri kwa kuanzia ile njia ya Machame KINAPA wajenge majiko ya kupikia na sehemu za kulia (dinning tent), hii itasaidia sana kuanza tu uniformity na kuzuia kila kampuni kuchimba sehemu tofauti kuweka mahali pa kulia na kupikia na hii itavutia sana watalii kwa kuona park fee wanazolipa zimetumika kwa kuendeleza park hiyo ukizingatia ilikusanywa zaidi ya bilioni 20 hizi ni Mlima Kilimanjaro tu.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kilimanjaro, Jimbo la Moshi Vijijini, Kata ya Mbokomu wenyeji waligundua mti mrefu sana na unakisiwa una ziadi ya miaka 500 mpaka leo sijaona juhudi zozote za Serikali kwenda kuhifadhi sehemu ile kuweka uzio ili watalii waanze kuutembelea officially na Serikali wanapeleka watalii pale anatoza asilimia ngapi kutokana na mti huu?