Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ukuaji na uingiaji wa watalii ulikuwa asilimia 12.9 mwaka 2015/2016; mwaka 2016/2017 mwaka wa kwanza wa Awamu ya Tano kasi imeshuka mpaka asilimia 3.5 tu. Hifadhi ya Ruaha inayopakana na wananchi maeneo ya Mbarali wapo katika wakati mgumu wa kufukuzwa kwenye makazi yao na mpaka sasa hakuna hata waliopata fidia yoyote mpaka sasa hawana cha kufanya.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ukataji wa miti kilometa za mraba 1,430 sawa na zaidi ya ukubwa mkoa mzima wa Dar es Salaam huu mradi si wa Watanzania kwa maana ya kuwasaidia. Tunaomba Serikali ichunguze na kuamua kwa faida ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, Guanzhuo ni mji wa kibiashara lakini hatuna Balozi Mdogo na timu ya kutangaza biashara hasa watalii kuja nchini kwetu kwani Kenya ina timu inayofanya matangazo ya nchi yao. Hakuna pesa za kutangaza utalii kwa nchi yetu na kutegemea makampuni binafsi ambayo hata wao hawaweki mkazo juu ya utalii huu. Vifaa vya kutendea kazi kwa wafanyakazi mbugani kama magari, tochi, bunduki hata boti sehemu zenye kuhitaji mabomu. Tunaomba Serikali iongeze bidii katika kuwezesha fedha za utendaji.

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Rungwe kuna vivutio vingi sana lakini hakuna uwekezaji wa kutosha ili kuvuta watalii maeneo hayo ni Daraja la Mungu, Lake Ngozi na Kijungu. Haya maeneo ni ya muhimu sana kwa uchumi wa Wilaya ya Rungwe tunaomba Serikali iwekeze maeneo hayo.