Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara, Mheshimiwa Waziri kwa utendaji na usimamizi mzuri katika kuhakikisha mali na rasilimali zetu za asili zinatunzwa na pia kukuza na kuinua sekta ya utalii nchini.

Mheshimiwa Spika, ushauri, katika kutekeleza nia njema ya Serikali kwa kuweka Mfuko wa Misitu, huoni vyema Wizara ikafuatilia kwa karibu zaidi juu ya wanufaika wa mfuko huo kama wanakidhi vigezo husika kwa lengo lililokusudiwa ili kuepuka wajanja kuitumia fursa hiyo na wale walengwa husika kukosa fursa ya kupata (fund) hizo kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, Serikali iendelee kuelimisha juu ya kulinda na kuhifadhi uoto wa asili. Mali Kale zitunzwe, zifanyiwe ukarabati na zilindwe ili ziweze kubaki kuwa ni urithi wetu wa Taifa kwa lengo la kuhifadhi historia na kuongeza vivutio vya utalii. Kuangalia namna ya kupata nishati mbadala yenye gharama nafuu kwa wananchi ili kuepusha ukataji wa miti kwa madhumuni ya kutengeneza nishati ya kuni na mkaa. Upatikanaji wa miti upewe mkazo wa pekee kunusuru nchi kuwa jangwa. Baada ya kupandwa kuwe na ufuatiliaji wa karibu kuhakikisha miti hiyo inakuwa vizuri.

Mheshimiwa Spika, ahsante naunga mkono hoja endeleeni kuchapa kazi kwa manufaa ya Watanzania.