Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Dkt. Hamisi A. Kigwangalla (Mb) pamoja na Naibu Waziri Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga (Mb) kwa kazi nzuri mnayoifanya katika Wizara ya Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali ijenge uzio wa senyenge katika hifadhi za mbuga zetu ambazo zinapakana na makazi ya wananchi ili kuepusha wanyamapori kutoingia katika makazi ya raia na kusababisha maafa hadi kupelekea kifo kwa wananchi. Pili, Serikali itafute matumizi ya mkaa mbadala ili kuepuka ukamataji wa mkaa unaotokana na misitu. Pia mkaa huo mbadala utaepusha wananchi kutokata miti hovyo na kuharibu misitu yetu na kupelekea ukame.

Tatu, naishauri Serikali iongeze vyuo ambavyo vitasaidia nchi kuweza kupata wataalam wa kutosha ili kusimamia maliasili yetu pamoja na kukuza utalii wetu.

Mheshimiwa Spika, Serikali iboreshe kiwanja cha ndege kilichopo katika Mkoa wa Morogoro Mjini ili kuweza kutumika nyakati zote za usiku na mchana ili kuwasaidia watalii ambao watakuja kutembelea mbuga ya wanyama ya Mikumi National Park kufika kwa urahisi. Pia Serikali iboreshe miundombinu iliyopo ndani ya mbuga zetu za wanyama na ili kuweza kurahisisha watalii kufika maeneo mbalimbali ndani ya mbuga kwa urahisi katika vipindi vyote vya msimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali iongeze magari ya kisasa ambayo yatatumika ndani ya mbuga zetu mara tu watalii wanapotaka kwenda kuwaona wanyama na vivutio mbalimbali. Pia nashauri kuutangaza mlima wetu wa Kilimanjaro kama kivutio cha watalii hususan kwa watalii wa nje ya nchi. Ili kuepuka nchi ya Kenya kutangaza mlima Kilimanjaro kuwa upo nchini mwao.

Mheshimiwa Spika, mwisho namuomba Mwenyenzi Mungu awape afya njema na umri mrefu ili kuweza kuwatumikia Watanzania.