Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Spika, nasikitika kuona vyanzo vya utalii vilivyopo Wilaya ya Mbozi zimesahauliwa kuwekwa kwenye kumbukumbu ya Wizara, pia havijatangazwa mfano katika Kata ya Nanyara Wilaya ya Mbozi kuna vivutio vya utalii vya maji moto na mapango ya popo. Vyanzo hivi havitajwi popote pale wala havipo kwenye kumbukumbu za Wizara. Wizara ichukue hatua thabiti za kuvitambua vyazo hivi na kuvitangaza ili kuongeza mapato ya Halmashauri ya Mbozi na Serikali Kuu.

Mheshimiwa Spika, pia askari wa wanyama pori waepukane na mauaji ya raia wanaoingia kwenye maeneo ya hifadhi badala yake wachuke hatua za kisheria na siyo kuua. Mfano wapo wananchi wasiokuwa na hatia waliuawa mwaka jana Arumeru, Arusha na maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.