Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. RUKIA KASSIM AHMED: Mheshimiwa Spika, tumekuwa na matatizo mengi hasa baina ya wakulima na wafugaji. Tatizo hili limekuwa sugu sana hasa kwa wafugaji kuwa na mifugo ndani ya nchi hii imekuwa ni shida sana. Wafugaji wanahangaika sana na mifugo, kila wanapoelekea wanafukuzwa na wakati mwingine mifugo yao inakamatwa na kupigwa mnada, wanalipishwa fedha nyingi sana ambazo hata uwezo wa kuikomboa mifugo yao hawa wanabakia na umaskini mkubwa, wengine wanapata mshituko wa moyo wanakufa. Serikali ilione tatizo hili kuwa ni kubwa na ipo haja ya kuingilia kati ili tuweze kuishi kwa amani na hawa wenzetu ambao ni wafugaji wajisikie kuwa na wao wanathaminiwa ndani ya nchi yao.

Mheshimiwa Spika, pia najielekeza kwa wakulima wetu wanapata shida sana wanapolima wakati mwingine wanabanwa wamelima kwenye hifadhi ya akiba. Hivyo basi Serikali yetu iwatengee eneo wananchi wetu waweze kulima isiwe kila eneo ambalo ni zuri kwa kilimo linawekwa kuwa ni kwa ajili ya hifadhi tu. Tuwasaidie wakulima wetu na wao wahisi kuwa wanathaminiwa na kupewa nafasi ya kuweza kujiendeshea maisha yao. Serikali itenge maeneo maalum kwa ajili ya kilimo.