Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na ninachangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo langu la Nkasi Kusini kuna Vijiji vya Kusapa, King’ombe, Mlambo, Kilambo, Ng’undwe, Namansi, Kizumbi na Mlalambo, vilevile Kijiji cha China na Kijiji cha Nkata mipaka ya vijiji vyao na hifadhi havieleweki na vijiji vingine viko ndani ya pori na kuwa pori lilikuta vijiji hivyo na kuvizingira, kwa hiyo hawana ardhi ya kutumia kwa ajili ya kuendeleza maisha yao ya kila siku.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali kupitia Kamati ya Wizara mbalimbali itoe matokeo ili kusuluhisha jambo hili. Naomba matokeo yawe wazi na wananchi wajue hatma ya jambo hili.

Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Kasapa kwa mfano, kimezingirwa na maeneo ya hifadhi mawili pori la TFS na Lwanfi Game Reserve ambapo Wizara ilitembelea kwa juhudi yangu. Waziri mstaafu Mheshimiwa Maghembe aliweza kuona jinsi wananchi walivyokosa eneo la kulima maana mipaka iko mita zisizozidi 300 pande zote nne yaani Mashariki, Magharibi, Kusini na Kaskazini. Wizara ilete mapendekezo ni namna gani Wizara imejipanga kuwasaidia wananchi baada ya kutembelea kila kijiji wamekaa kimya, why?

Mheshimiwa Spika, matatizo ya wanyama (tembo) wanasumbua wakulima wa Vijiji vya King’ombe, Mlalambo, Ng’undwe na Mlalambo na Vijiji vya Kisumbaka na Kasanga Wilayani Kalambo, tembo wameuwa watu zaidi ya watatu kwa miaka miwili mfululizo. Wananchi wa eneo hilo wanasema hawana mtumishi hata mmoja wa kuzuia tembo wasilete maafa hayo. Tunaiomba Serikali ipeleke watumishi wa Maliasili Kisumba kuzuia maafa haya. Naiomba Serikali itusaidie kupunguza ukubwa wa pori hili ili wananchi wa vijiji nilivyovitaja wapate ardhi ya kulima ili waendeleze maisha yao hapa duniani.

Mheshimiwa Spika, Mlalambo, Ng’undwe wananchi wanapekuliwa hovyo hovyo, hawawezi kujenga nyumba eti mbao kutoa wapi? Wananchi wanachapwa viboko, Mlalambo na Ng’undwe si sawa eti huo ubao wa mlango katoa wapi? Haya ni malalamiko niliyopewa nilipoenda kwenye ziara, naomba tuliangalie jambo hili.

Mheshimiwa Spika, kuna ardhi ya wananchi ya Kakumbu inatumika chini ya kiwango iko wapi Kamati ya Wizara tano ambayo tumeipatia migogoro ya watu wa Sintali, Nkama na Nkomanchindo.