Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, kuna mkakati gani uliowekwa na Serikali kuhakikisha kuwa miji mikongwe inatangazwa na kukarabatiwa ili iwe kivutio cha utalii kwa mfano Mji wa Mikindani katika Manispaa ya Mtwara, Mikindani umetekelezwa, mchafu, miundombinu mibovu na kadhalika. Naamini mji ule ukiendelezwa na kutangazwa vizuri utawavutia watalii hivyo kuongeza pato la Manispaa na Taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, Serikali ina makakati gani wa kuhakikisha inautangaza na kuuendeleza utalii wa bahari na fukwe zake. Wananchi wanaoishi maeneo yenye bahari mfano Mtwara, tulitarajia kuwa Serikali ingefanya uwekezaji mkubwa katika fukwe za bahari kwa kushirikiana na wawekezaji wengine ili kuwezesha uchumi kukua maeneo husika. Kinyume chake fukwe hizi zimeachwa chafu bila uwekezaji wowote. Je, Serikali inaridhika na hali hii?

Mheshimiwa Spika, naomba kujua msimamo wa Wizara hii juu ya kutoa elimu mbalimbali zinazohusu uhifadhi wa watu na wanyama pori ambavyo vimekuwa vikitekelezwa na watu mbalimbali ikiwemo Serikali mfano kibali cha kukata miti mingi sana katika mbuga ya Selous.