Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, na mimi naunga mkono hoja hii ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Pamoja na kuunga mkono, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa niaba ya Rais kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuhakikisha anasimamia vizuri sekta hii ya maliasili na utalii na hata kuleta tija nzuri katika Taifa.

Mheshimiwa Spika, Waziri alipata nafasi ya kutembelea mbuga na hifadhi zetu katika Halmashauri ya Chalinze na Wilaya ya Bagamoyo. Katika ziara hiyo amejionea mengi ikiwemo migogoro baina ya wananchi na hifadhi. Lakini pamoja na maelekezo, hakuna lililofanyika hadi leo. Wananchi wameendelea kupata shida na Serikali Kuu imekuwa kimya.

Mheshimiwa Spika, ni masikitiko yangu kuwa mbuga ya hifadhi au Pori la Hifadhi la Uzigua na Wami Mbiki limekuwa sehemu nzuri kwa ajili ya mapitio ya wanyama. Lakini ujangili umekuwa shida, pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali sijajua mna mipango gani kuhusu usimamizi wa WMA hii.

Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri amezungumzia juu ya uangalizi wa maeneo ya malikale. Pamoja na mipango mizuri, lakini ukweli ni kwamba Mji wa Bagamoyo ambao ndani yake kuna Caravan Serai na Mapango ya Kaole umesahaulika. Mji huu una mambo mengi ya kihistoria na majengo mengi ya kale. Kwa kifupi matarajio yangu ni Serikali kuwa na mkakati juu ya mji na historia wa Bagamoyo. Inakumbukwa katika maeneo mengi kuanzia ujio wa Wareno, Wajerumani, Waarabu na shughuli za utumwa, bandari ya kwanza Tanzania na mengineyo mengi lakini Bagamoyo mmeisahau.

Mheshimiwa Spika, Waziri atakapokuja atusaidie sisi wana wa Bagamoyo kufahamu nini kinafanyika au mpango gani uliopo juu ya Mji wa Bagamoyo.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.