Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia Wizara hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, maliasili na utalii kuweka mipaka ya hifadhi ya uwanda iliyowekwa toka mwaka 1959, eneo lililotolewa na wakulima, lakini kwa sasa ramani hiyo imekiukwa na kuingilia makazi ya wananchi katika mipaka ya Vijiji vya Kilangawana, Maleza, Kilyama, Tundu, Legeza, Kapenta, Mkusi Iwelya Mvua na Nankanga. Nataka Mheshimiwa Waziri anipatie majibu kwa hoja zifuatazo:-

(a) Hifadhi ya Uwanda, je, ni mali ya Maafisa Misitu wa Mkoa wa Rukwa?

(b) Kwa nini hifadhi hiyo imejaa mifugo mingi hata uthamani wa hifadhi haupo tena?

(c) Kwa nini wanaingiza mifugo (ng’ombe) kwa kuwatoza pesa kwa manufaa binafsi?

(d) Kwa nini wanaruhusu wakulima ndani ya hifadhi hiyo baada ya mpunga kukomaa wanavuna wao kwa kutumia ukatili wa kinyama kabisa? Naomba nipatiwe majibu katika hoja hizi vinginevyo sitaunga mkono hoja na nitashika shilingi ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili.