Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na maoni ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwamba kumekuwa na ushirikishwaji mdogo sana na wananchi katika uwekaji wa vigingi vya mipaka ya hifadhi/vijiji.

Mheshimiwa Spika, zoezi la utambuzi wa mipaka katika Wilaya ya Malinyi katika Pori Tengefu la Kilombero limekamilika lakini limeacha changamoto/lawama kwa Serikali kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa mapana. Matokeo ya zoezi hili limesababisha wananchi kukosa mashamba na baadhi ya vitongoji kuwa katika miliki ya pori tengefu. Hii imeleta taharuki kubwa kwa wananchi kukosa ardhi kwa maendeleo ya kilimo na kiujumla ustawi wao.

Mheshimiwa Spika, katika kampeni zake Mheshimiwa Rais mwaka 2015 aliwaahidi wananchi wa Malinyi kuongezea ardhi kutoka katika kingo (buffer zone) ya Pori la Kilombero. Kingo hii bado ni pana sana (kilometa 5 -12) hivyo kuwaongezea wananchi angalau kilometa tatu tu hakutoathiri kwa vyovyote ustawi au uendelevu wa Pori Tengefu la Kilombero. Hali hii kwa ukosefu wa mashamba kwa wananchi wengi wa Malinyi kutakuwa na athari kubwa kimaendeleo, ustawi wa uhai kiujumla kwa wananchi wa Malinyi.

Mheshimiwa Spika, ninaiomba Wizara ya Maliasili na Utalii iridhie maoni/ushauri wa Kamati hususan kurejea upya mipaka ya Pori Tengefu la Kilombero kunusuru mashamba na baadhi ya vitongoji na kuondoa migogoro katika maeneo hayo. Ahsante.