Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, uhifadhi wa Ziwa Manyara; ziwa hili ni miongoni mwa maeneo ya utalii hapa nchini kwa watalii wengi kutembelea. Hata hivyo, ziwa hili lipo kwenye hatari ya kupotea/kutoweka kutokana na tope lililojaa ziwani kunakosababishwa na shughuli za kilimo katika maeneo yanayozunguka ziwa. Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka kuokoa Ziwa Manyara ambalo ni kivutio cha utalii hapa nchini?

Mheshimiwa Spika, kuhusu tozo nyingi katika hoteli za kitalii; tunapohitaji sekta ya utalii iendelee kukua na kuongeza pato la Taifa ni muhimu na ni lazima kuhakikisha kunakuwa na mazingira mazuri na rafiki kwa wawekezaji katika sekta hii ya utalii. Hoteli za kitalii zimekuwa zikilipa tozo nyingi sana hivyo kufanya hoteli hizi kuwa na mazingira magumu kuendesha biashara.

Ushauri, Serikali itazame kwa upya tozo hizi ili kuendelea kuwajengea mazingira mazuri wawekezaji.

Mheshimiwa Spika, TALA ni leseni inayotolewa kwa makampuni ili waweze kuendesha shughuli za utalii. Hata hivyo leseni hii imekuwa ikilipwa na/au kutolewa kwa mtu akiwa na magari matatu kwa kulipa dola 2,000. Hata hivyo, mtu akiwa na magari zaidi ya matatu analazimika kulipa sawa na mwenye magari matatu (kwa kuwa ni takwa la kisheria). Hivyo basi, mtu akiwa na magari 50 au 100 atalipa sawa na mwenye magari matatu. Hapa hakuna usawa na ni unyonyaji kwa watu na kuendelea kuweka mazingira magumu kwa vijana wanaotaka kujiajiri.

Mheshimiwa Spika, ushauri, Serikali itoze leseni hii kwa kila gari, kwa kufanya hivi Serikali itaongeza mapato na kutawapa vijana nafasi/fursa ya kuingia katika sekta ya utalii na kujiajiri.