Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watumishi wa Wizara kwa jitihada nzuri za kusimamia sekta ya utalii na shughuli zote za Wizara.

Mheshimiwa Spika, ushauri, takwimu za mchango wa sekta kwenye pato la Taifa (17%) na rate ya ukuaji ya number of arrivals kwa mwaka (3.3%) haziridhishi. Tanzania ina unique comparative advantage za kijiografia ambazo bado lazima ziwe optimized ipasavyo. Vikwazo ninaviona ni viwili.

Mheshimiwa Spika, kwanza Benchmark Tax Region ya sekta ya utalii against nchi washindani wetu. Findings za benchmarking zisaidie Wizara kukaa na Wizara nyingine zinazohusika (mfano Wizara ya Fedha, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji na Ofisi ya Makamu wa Rais) na kujadili kwa pamoja ulazima wa kuboresha tax region ya sekta kuongezeka competitiveness.

Mheshimiwa Spika, strategy, Wizara iache mazoea ya kutegemea TTB pekee kufanya promotion marketing. Angalia nchi nyingine zilizofanikiwa wametumia modality zipi kufanya promotion and marketing.

Mheshimiwa Spika, naomba vigingi vilivyowekwa kwenye vijiji vya Mgoruka, Rweizinga zoezi lirudiwe upya na kushirikisha wananchi pamoja na mimi Mbunge ili kuleta ustawi mzuri na ujirani mwema kati ya wananchi wangu na mapori akiba ya Kimisi na Burigi.

Mheshimiwa Spika, kaeni na Ofisi ya Makamu wa Rais na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji muangalie namna ya kushirikiana ili kutumia teknolojia ya majiko jadidifu kama mbadala wa utumiaji wa mkaa. Kutumia mabavu kukataza utumiaji mkaa si sustainable na ni ishara ya kukosa innovation na mikakati ndani ya Serikali.