Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Spika, migogoro kati ya hifadhi za wanyama na vijiji vinavyozunguka hifadhi hizo ni ya muda mrefu na inaumiza sana. Mgogoro kati ya Vijiji vya Losilete, Upper Kitete, Slahamo, Makuromba na Endamaghang Wilayani Karatu na Hifadhi ya Ngongoro ni ya muda mrefu. Pia mgogoro kati ya TANAPA (Lake Manyara National Park) na wananchi wa kata ya Buger umekosa wa kusuluhisha.

Mheshimiwa Spika, askari wa wanyamapori wamekuwa na ubabe wa kuwanyanyasa na kuwapiga wananchi. Mipaka ya hifadhi hizi imewekwa siku nyingi tangu ukoloni na bila kumung’unya maneno mipaka halisi inafahamika, inaonekana na ni ubabe tu wa hifadhi kuyaongezea maeneo ya wananchi. Serikali iachane na tabia ya kuvamia maeneo ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, wanyama wamekuwa chanzo cha kutia umaskini wananchi wetu. Tembo na mbogo wamekuwa wakitoka hifadhini na kwenda vijijini kuharibu mashamba ya wananchi na hata kusababisha vifo. Uongozi wa hifadhi hizi hauko makini kuwazuia wanyama hao. Niishauri Serikali kuhakikisha timu za doria zinaongezwa na kupewa zana za kuwadhibiti wanyama hao.

Mheshimiwa Spika, sheria ya kutoa kifuta jasho na pole kwa uharibifu na mauaji yanayofanywa na wanyama hao imepitwa na wakati na inahitaji marekebisho makubwa. Pole ya shilingi 1,000,000 haitoshi kabisa hivyo inafaa iongezwe.

Utaratibu wa kukamata na kutaifisha mifugo ya wafugaji pale inaposemekana wameingia hifadhini haufai kabisa na ni unyanyaswaji wa wananchi. Ng’ombe wamekuwa wakitaifishwa kwa uonevu mkubwa. Utaratibu huu ubadilishwe, haufai kabisa.