Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, ningependa kuchangia mambo machache katika Wizara hii ya Maliasili na Utalii. Jambo la kwanza ni kuhusu mtiririko wa bajeti katika Wizara hii. Mwaka 2016/2017 Bunge liliidhinisha fedha za miradi ya maendeleo kiasi cha shilingi 17,746,682,000; hata hivyo, kiasi kilichotolewa ni shilingi 2,199,870,358 ambacho ni sawa na asilimia 12 ya fedha zote zilizotengwa.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2017/2018 jumla ya shilingi 51,803,204,000 zilizoidhinishwa na Bunge kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo mpaka kufikia mwezi Februari, 2018 Wizara ilikuwa imepokea jumla ya shilingi 27,946,781,302 ni ambayo ni sawa na asilimia 54 ya fedha zilizoidhinishwa. Makadirio ya bajeti ya mwaka 2018/2019 ni shilingi 29,978,082,000 hii inaonesha anguko la bajeti ya Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, mtiririko wa bajeti wa Wizara hii unaonesha bajeti ya maendeleo imekuwa ikitegemea fedha za nje. Mfano kwa mwaka 2017/2018 fedha za ndani zilizotolewa zilikuwa shilingi 11,353,250,489 na fedha za nje ni shilingi 16,593,530,813. Mwaka wa fedha 2018/2019 fedha za maendeleo zinakadiriwa kwa shilingi 29,978,082,000 kati ya hizo fedha za ndani ni shilingi 3,000,000,000 tu.

Mheshimiwa Spika, hili ni tishio kubwa kwa Wizara kwani kuzidi kutegemea misaada kutoka kwa wahisani hakuwezi kamwe kunyanyua sekta hii. Kumekuwa na matamko mbalimbali ya Mheshimiwa Rais, hatutategemea wahisani, ila hali halisi ni kuwa bajeti yetu imekuwa tegemezi kwa zaidi ya asilimia 50. Hii inaonesha kuwa bado Serikali haijakubali kuwekeza ipasavyo kwenye sekta ya maliasili na utalii.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni kuhusu ukuaji wa sekta ya utalii nchini. Mwaka 2012/2016 wastani wa ukuaji wa sekta ya utalii ilikuwa asilimia 13.7 mwaka 2017 sekta ya utalii imekuwa kwa asilimia 3.3 kwa sababu ya maamuzi holela ya Wizara hii, unstable policy decisions katika sekta ya uwindaji ambayo imesababisha kushuka sana kwa ukuaji wa sekta ya utalii.