Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. ZITTO R. Z. KABWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na kutokana na muda nimewasilisha kwa Mheshimiwa Waziri maelezo ya mchango wangu katika maeneo mbalimbali ambayo nachangia ili tuweze kupata majibu ya Serikali. Kwa hiyo, nitachangia maeneo machache tu kutokana na muda ambao umepatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, nchi yetu ilijenga heshima kubwa duniani siyo kwa sababu ya utajiri, siyo kwa sababu ya idadi ya watalii ambao tunao bali ni kwa sababu ya kupigania utu mahali popote pale duniani. Mwaka 1961 wakati tunapata uhuru, usiku wa kuamkia siku ya uhuru tuliweka Mwenge juu ya Mlima Kilimanjaro na Mwalimu Nyerere alitamka maneno yafuatayo:- (Makofi)

‘Tunataka kuwasha Mwenge na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete matumaini pale ambapo hakuna matumaini, upendo pale palipo na chuki, heshima pale palipojaa dharau.’ (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huu ndio umekuwa msingi wa sera yetu ya mambo ya nje miaka nenda miaka rudi. Ndio mambo ambayo Waziri Mahiga, amekuwa akifundisha, ametumikia nchi yetu, amekuwa Balozi wa Umoja wa Mataifa lakini leo mambo ambayo yanatekelezwa tunashindwa kuelewa kabisa kama ni Mheshimiwa Dkt. Mahiga huyu tunayemjua au kuna Mheshimiwa Dkt. Mahiga mpya baada ya kuwa Waziri wa Mambo ya Nje. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimetazama kura zote UN Security Council, wakati Waziri Dkt. Mahiga anaiwakilisha nchi yetu. Kura zote zilizokuja kupigania wanyonge tulikuwa pamoja na wanyonge, lakini toka mwaka 2016 kura zote tunazopiga kwenye majukwaa ya kimataifa uanzie UNESCO Parish, mwezi Oktoba, 2017 na mpaka hivi majuzi ama tuna abstain tunaona aibu kusimama na wanyonge au tunapiga na watu ambao wanawakandamiza watu wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna mtu anayekataza nchi yetu kuwa na mahusiano ya kibalozi na Israel. Hata Mwalimu Nyerere hakukataza kuwa na mahusiano na Israel lakini Mwalimu Nyerere alisema kwamba mahusiano hayo yasitufanye tuache kusimamia wanyonge. Mheshimiwa Waziri alikuwa Israel juzi, amekwenda Israel at the time, ambayo ndio inawaumiza Wapalestina kuliko wakati mwingine wowote miaka 70 ya Taifa la Israel. Amekwenda kutembelea miji ambayo inapakana na Gaza, kulikuwa na massacre. Nchi yetu leo inaona aibu kulaani mauaji ya watu wanyonge wanaokandamizwa, walionyang’anya ardhi yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma maelezo ya Wizara ukurasa wa nane mpaka wa tisa, propaganda kutaka kuridhisha watu ambao bado wanaamini misimamo ya Mwalimu Nyerere kwamba bado tuna misimamo hiyo, lakini ukitaka kujua hasa nini misimamo ya Serikali kwenye mambo ya kimataifa nenda angalia ukurasa wa 51 mpaka 60 ya hotuba ya Mheshimiwa Waziri. No mention of Palestina, no
mention of POLISARIO, Ame-mention kwenye preamble huku ili kuturidhisha kwamba misimamo yetu haijabadilika, lakini huku amekuja kuzungumzia mpaka mambo ya North Korea huko, nothing about watu ambao tumekuwa tukiwapigania.

Mheshimiwa Naibu Spika, juzi watu ambao tumewakomboa South Africa, baada ya massacre ya Gaza, wamemwondoa balozi wao, Waziri wetu anakunywa mvinyo na Netanyahu, the butchery ya Wapalestina. Anaenda kwenye television za Israel, television za Taifa anapongeza Israel, anashindwa kutoa neno moja la kulia na watu ambao, sasa mambo yote aliyokuwa anafundisha Mheshimiwa Dkt. Mahiga siku zote ya foreign yanaenda wapi? At this age anavunja heshima yake yote ya huku nyuma. Kwa sababu ya nini misaada ya Israel? POLISARIO, its true, amezungumza rafiki yangu Mheshimiwa Cosato kwamba Algeria wana ubalozi wana… mwisho. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)