Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Vilevile niungane na wenzangu wale ambao walimpongeza ndugu yetu Sugu kwa kuweza kurudi hapa Bungeni, baada ya kutoka kifungoni kule Mbeya. Pia tumshukuru Rais kwa kuliona hilo na kuweza kuleta tafifu ya kumrudisha hapa na leo tunaye. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo nataka kusema kwa haraka haraka kulingana na muda suala la kwanza, Tanzania ndani ya tasinia ya Afrika mashariki. Kila tunapokwenda bado hakujawa na mikakati chanya ya kuweza kukabiliana na ushindani iwe wa uchumi, elimu, hata utamaduni. Tunahitaji Wizara ieleze kwa undani ni mikakati gani ambayo itaweze kutufanya sisi kama nchi kuweza kukabiliana na tasinia ya ushindani ndani ya East Africa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaona wenzetu kila siku wanafungua fursa nyingi za kiuchumi katika maeneo yao, lakini bado pamoja na harakati ya miradi ambayo iliyoko ndani ya nchi ya Tanzania haionyeshi competitive advantage ya kuweza kushindana na wenzetu ambao wako katika maeneo yetu wakati sisi tuna rasilimali nyingi ambazo zinaweza kutupaisha haraka zaidi kuliko wao. Kwa hiyo, nimwombe Waziri aje atupe maelezo hapa mkakati gani tunao ndani ya utengamano huu wa East Africa, kukabiliana na ushindani wa kibiashara, ushindani wa kielimu lakini vilevile na kiutamaduni baina ya nchi zetu hizi sita zilizo katika mtengamano huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo nataka kulizungumza ni suala zima la Balozi zetu zilizo nchi za nje. Bado uwezo wa Mabalozi kuona output katika nchi hii ni mdogo. Tegemeo la kupewa post hizi hawa Mabalozi tunategemea waitangaze hii nchi kwa vivutio mbalimbali vya kiuchumi, kiutamaduni na teknolojia vilivyoko ndani ya nchi hii. Hata hivyo, tumeona tu wenzetu Wafaransa juzi balozi amechangamka na kuweza kuleta delegation hapa ya Wafaransa kuja kuangalia fursa za uwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, na sisi Tanzania tunahitaji kuona tunatoa delegation mbalimbali zinakwenda katika nchi mbalimbali kuangalia fursa. Siyo hao tu wafanyabiashara hata nao Wabunge pia wapewe fursa za kwenda nje kuangalia fursa mbalimbali za kiuchumi, kiutamaduni na teknolojia ili waweze kuisemea nchi hii na kuleta matunda ambayo yataweza kuisaidia hii nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna vitu vingi ambavyo tunaweza kufanya uwekezaji, lakini tuna miradi mingi ya kimkakati ambayo inaweza kuitoa nchi hii, lakini tunasema miradi hii tumeifungasha sisi wenyewe tu. Wazo langu tuitoe, tuitangaze kama tunaanzisha mradi mkubwa wa Stiegler’s Gorge, tuutangaze duniani utapata support, watu wanahitaji kuuona na kuujua, ziletwe ripoti za hii miradi ili tuweze kuona miradi hii inapata ufadhili, lakini vilevile inapata…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)