Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, usalama wa Watanzania wanaoishi nchi za nje, suala hili limekuwa na changamoto kubwa sana kwa Watanzania wenzetu wanaojishughulisha na mambo mbalimbali ikiwemo kutafuta kazi za ndani na masuala mbalimbali yanayohusiana na biashara. Wanapopata matatizo wanaobeba jukumu ni ndugu zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutumia diplomasia kwa wafungwa kwenye magereza zilizopo nje ya nchi kuwaomba waje watumikie kifungo kwenye nchi yao kwa maana ya Tanzania ili kuendelea kujenga ushirikiano mzuri. Kutumia balozi zetu kunufaisha Taifa letu. Serikali ifuatilie kwa karibu utendaji wa Mabalozi na kuwapa semina elekezi kwa kutazama uhitaji wa Taifa letu kwa wakati huo na kuwakumbusha wajibu wao ili Taifa letu liweze kunufaika.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la diplomasia ya uchumi; jambo hili ni vyema likapewa kipaumbele kwa kuwa Taifa letu bado linakua na kujenga ukaribu kwa mataifa ambayo ni marafiki zetu ili kukuza uchumi wa Taifa letu. Kutumia diplomasia Serikali itumie fursa hiyo kutafuta masoko ya mazao ya biashara. Suala hili halijatunufaisha kama Taifa kuwa na manufaa ni pale ambapo tutatumia nafasi hiyo inapotokea na ziada ya kutosha na tukawa na ziada.

Mheshimiwa Naibu Spika, lugha ya Kiswahili, suala hili tumelizungumza sana, nashauri Serikali kupitia diplomasia kushawishi nchi marafiki kutumia lugha ya Kiswahili ambayo itasaidia kwa Taifa letu kwa wakufunzi ambao watakuwa Watanzania na kama Taifa tutanufaika kwa kupata ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutumia Ziwa Tanganyika, Victoria na Ziwa Nyasa kwa kuwa mazingira haya kushirikiana katika uvuvi ni vyema kama Taifa tukawa na uvuvi wa kisasa utakaoleta tija kwa Taifa letu badala ya kuchoma nyavu zetu za wavuvi. Kutumia Watanzania wanaoishi nje ya nchi kunufaisha Taifa letu. Tukiwatumia vizuri Watanzania hawa katika biashara na katika elimu tutapata manufaa makubwa hasa pale ambapo na wao watatambua kuwa Taifa linatambua uwepo wao kule waliko.

Mheshimiwa Naibu Spika, waliopelekwa kusoma nje ya nchi, Serikali kupitia ubalozi watumie nafasi zao kushawishi na kuomba wanafunzi hawa kupunguziwa ada au kufutiwa kabisa ili kuwatia moyo wazazi na walezi ambao wamejitolea kuwapeleka watoto au ndugu kusoma nje ya nchi kwani ni kwa manufaa ya nchi nzima.