Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefikia wapi juu ya suala la mpaka eneo la Ziwa Nyasa baina ya nchi yetu na Jamhuri ya Malawi. Suala hili limekuwa ni la muda mrefu sana na hakuna ufumbuzi uliofikiwa juu ya suala hili la mpaka. Naomba kufahamu suala hili limefikia wapi? Naomba Mheshimiwa Waziri wakati anahitimisha mjadala tupate ufafanuzi wa kina juu ya mahali walipofikia katika maamuzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya ya Ludewa ambayo imepakana kwa eneo kubwa na nchi ya Malawi kuliko Wilaya za Kyela na Nyasa lakini hatuna customs ambazo zingerahisisha kwa watu wanaosafiri kwenda Malawi badala ya kupitia Kyela ambako ni mbali na kunaleta usumbufu mkubwa kwa wananchi wanaotaka kusafiri kibiashara na kushindwa kulitumia soko la nchi jirani. Wilaya ya Ludewa ni eneo zuri kwa uzalishaji wa mazao ya biashara kama mahindi, maharage, chai, pareto, alizeti na kadhalika. Kuna umuhimu wa kuwa na bandari na TRA kurahisisha mienendo ya watu na bidhaa.