Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Wizara hii muhimu niwatakie masuala yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Israel, sera yetu ya mambo ya nje siku na katika Awamu zote Nne zilizotangulia, zilikuwa rafiki wa kweli wa Israel na Palestine. Awamu ya Tano imefungua Ubalozi kwa mbwembwe zote Israel. Je, wanajua mlivyoikwaza the Arab World!

Mheshimiwa Naibu Spika,Morocco/Western Sahara, awamu hii imefungua Ubalozi Algeria. Hii ni sawa, lakini wakati huo huo wanafunga ndoa ya rafiki na unafiki na Morocco. Algeria ndiyo mtetezi wa Sahara Magharibi. Mbinu zetu za ukombozi zimeishia wapi? Morocco ilikuja mwaka jana na kuweka mikataba 21, iko wapi sasa? Waziri atueleze mikataba yote imefika wapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, najua hamna kitu, Mfalme wa Morocco alikuja kwa nia ya kuishawishi Serikali iunge mkono azimio la ombi la Morocco kurejea AU na siyo vinginevyo. Mengine yote yalikuwa danganya toto. Mbaya zaidi ukikutana na watu wa Morocco utasikia Dkt. Mahiga mtu wetu, Dkt. Mahiga mtu wetu. Sasa hapa ni Dkt. Mahiga au ni Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, ushiriki hafifu wa nchi katika mikutano ya kimataifa na kimkakati. Safari za nje kwa Mheshimiwa Rais kuzikatisha amechemsha, Watanzania sasa lazima tumlazimishe Mheshimiwa Rais kuhudhuria mikutano muhimu. Mwaka huu tumlazamishe aende UN akahutubie Umoja wa Mataifa tufurahi kwa kuwakilisha nchi yetu na kupata fursa mbalimbali. Haiwezekani Mheshimiwa Rais awe ametembelea Rwanda na Uganda tu miaka yote hii, tukiuliza tunaambiwa ni kubana matumizi, hapana! Siyo kweli. Ikulu na Wizara ituambie tu ukweli, kuna tatizo gani? Je ni lugha? Kama ni lugha si atumie Kiswahili tu kwanza atakuwa anakuza na kuitangaza lugha yetu. Je, ni afya? Je, ni usalama wake anahofia au ni majukumu? Katika haya yote sioni sababu labda kama ni ya kiafya.

Mheshimiwa Naibu Spika, msiba wa Winnie Mandela, kwenye msiba huu katika nchi yenye mahusiano mazuri ni sisi tangu enzi hizo hatukuweza kupeleka mwakilishi. Ajabu nchi zote za SADC zilituma wawakilishi, sisi Tanzania hatukwenda! Hii ni aibu sana!

Mheshimiwa Naibu Spika, je, kuna economic diplomacy tena nchini? Ipi! Hakuna economic diplomacy, sasa kuna diplomasia ya miundombinu tu, ambayo ni diplomasia ya barabara na Bombadier!

Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi amesikika akisema kuwa kwenye vikao mbalimbali inapofika zamu ya Tanzania kuongea basi watu wote walikuwa wanaacha kwenda hata chooni, walikuwa na shauku ya kusikiliza. Sasa ni kinyume chake, sasa hawana shauku na kwa kweli hakuna cha kusikiliza. Tumefika hapo? We are a laughing stock! Gone are the good days. Inachosha sana leo Bungeni tumeshangilia nafasi walizopata wenzetu kwenye Bunge la Africa (PAP). Tumeshuhudia si Mheshimiwa Rais tu haudhurii bali hata Mawaziri na mbaya zaidi Wabunge katika mikutano ya jimbo ambayo ni calendar meeting, hii sio sawa.