Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Ofisi za Balozi zetu, nashauri Serikali kujenga Ofisi zake katika Balozi zetu kwani fedha nyingi zinatumika kugharamia Ofisi hizi wakati kuna viwanja. Mfano, Msumbiji kuna eneo la kujenga na tunashindwa kujenga. Tukope hata mikopo ya masharti nafuu ili ije ilipwe kwa fedha zile ambazo tungelipa kodi ya majengo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, uteuzi wa Mabalozi; nashauri Serikali kuangalia uteuzi unaofanyika kama unaendana na faida tunazopata kutokana na uwekezaji huo katika Balozi hizo. Ni kwa kiasi gani upimaji wa utendaji wa Balozi zetu ukichukulia kuwa kuna malengo mahususi ya uanzishaji Balozi hizo ikiwa ni pamoja na kutangaza vivutio vya Tanzania ili kuwezesha Tanzania kupata wawekezaji.