Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Ahmed Mabukhut Shabiby

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gairo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naunga mkono hoja kwa hotuba hii ya 2016. Kwa vile Hotuba ya Waziri mpya na Awamu mpya ya Tano, lakini uhalisia Wizara hii. Umuhimu wa Wizara hii kwa miaka mingi sasa imekuwa haina msaada kwa wakulima hasa wa Mkoa wa Morogoro na zaidi Wilaya ya Gairo. Wilaya ya Gairo ni moja ya Wilaya zinazolima sana nchini pamoja na kuwa haipo kitakwimu na umaarufu cha ajabu Wilaya hii haipati ruzuku za pembejeo na ikipata zinakuja nje ya muda wa kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, mwaka huu mbegu imekuja mwezi wa Kwanza katikati, wakati kilimo cha Gairo mbegu inatakiwa mwezi Novemba. Gairo ina Tarafa mbili, Tarafa ya Gairo na Nongwe, Tarafa ya Nongwe yote ina maji ya kutosha, mito ya kudumu mingi, lakini hakuna mpango wowote wa kuendeleza kilimo cha umwagiliaji katika maeneo haya pamoja na Halmashauri ya Gairo kuomba pesa, lakini imekuwa haipewi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama tuna nia ya kuondoa nchi katika matatizo ya chakula na mazao ya biashara, wataalam wa Wizara wajiongeze na kujua kila sehemu inayofaa kwa kilimo. Siyo kunakili kila siku kuwa maeneo fulani ndiyo wanafaa au yanafaa kwa kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukija upande wa mifugo Wilaya hii ina mifugo mingi lakini kuna uhaba wa mabwawa ya maji kwa ajili ya mifugo, hasa katika Vijiji vya Kitaita, Ngayaki, Chogoali, Misingisi, Mkalama, Meshugi, Ndogomi, Kumbulu, Chilama. Tunaomba sana huduma hii ya mabwawa ichukuliwe kwa jicho la huruma na haraka, kwani wafugaji hawa wanapata tabu sana kwenda zaidi ya kilomita kumi hadi kumi na tano kwa ajili ya maji na mara nyingine wasipate maji ya kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, nategemea mtashughulikia suala hili.