Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Nishati

Hon. Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Nishati

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii ya kuweza kuchangia katika Wizara hii ya Nishati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri wote tunatambua kwamba kwa muda mrefu sana nchi yetu ilisemekana kukosa chanzo cha uhakika cha kuzalisha umeme baada ya mabwawa ya Kidatu na Mtera kupungukiwa na maji mara kwa mara, hali iliyosababisha kukosa umeme wa kutosha nchini. Kutokana na hali hii, Serikali iliyokuwa madarakani kwa kipindi hicho iliwekeza nguvu nyingi sana kwenye mradi wa gesi ambao ndiyo tulitegemea uweze kutuzalishia umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ya Nishati ilituhakikishia kwamba mradi huo ungeweza kutupatia umeme wa kutosha nchi nzima na hata tungeweza kuuza umeme kwenye nchi za jirani. Mradi huu wa gesi uligharimu takribani dola bilioni 1.225, katika dola hizo dola milioni 875.7 zilitumika katika ujenzi wa bomba la gesi ambapo takribani dola milioni 300 zilitumika katika ujenzi wa vinu kwa ajili ya kuchakata gesi. Leo hii Serikali inakuja na mradi mpya wa Stiegler’s Gorge. Mbali na kwamba mradi huu una madhara mengi yakiwemo yanayoweza kujitokeza kwenye mazingira yetu, lakini Serikali imeendelea kupigia debe huu mradi uweze kutekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wa CCM siyo kwamba sisi tuna akili mgando, Wabunge hatukatai maendeleo, miradi ya maendeleo tunaikubali, lakini ikumbukwe kwamba muda mfupi uliopita Serikali iligharamia mabilioni ya fedha ambazo ni fedha za walipa kodi wa Tanzania. Leo hii huu mradi unaenda kutelekezwa tunaingia kwenye mradi mwingine, tunaelekea wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiangalia katika mwaka wa fedha 2018/2019, pesa ambayo inaombwa kwa ajili ya Wizara ya Nishati ni Sh.1,665,141,000,000. Katika pesa hizi ambazo zinaelekezwa katika huo mradi ni shilingi bilioni 700 ambayo ni sawa na asilimia 42 ya fedha za miradi ya maendeleo katika Wizara hiyo ya Nishati. Vilevile pesa nyingine inayoenda ambayo ni Sh.112,083,000,000 zinzelekezwa katika mrai wa REA, ni asilimia 6 tu ndiyo iliyotengwa kwa ajili ya mradi huu wa gesi ambao tayari ulishagharimu pesa nyingi za nchi hii, hii maana yake nini? Mnataka kutuaminisha kwamba Serikali ina fedha nyingi au ni misuse ya zile resources chache tulizonazo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Stiegler’s Gorge itaenda kugharimu fedha hizi zote, wapi tunapoelekea? Tunawaambia nini wananchi wa Lingoko, Mkoa wa Lindi, wananchi wa Songosongo Kilwa, wananchi wa Mtwara Vijijini ambao wameacha makazi yao, wameacha mashamba yao kwa ajili ya kupisha mradi huo wa gesi ambao sasa hivi umeenda kupewa asilimia 6 tu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni suala ambalo kusema ukweli naishauri Serikali kuliko kuelekeza hii pesa katika mradi mpya huu wa Stiegler’s Gorge bora hiyo pesa ielekezwe katika mradi ambao tayari umeshaligharimu Taifa mabilioni ya fedha, haiwezekani kila siku tukawa tunaanzisha miradi mipya ambayo haitekelezeki. Mpaka leo hii fedha zilizotumika hatujaona returns zozote, leo hii tunaingia kwenye mradi mwingine? Waziri wa Nishati tunaomba mliangalie tena hili suala. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo napenda kuliongelea ni juu ya usambazaji wa gesi.