Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Nishati

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Nishati

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kwa kumpongeza Waziri, Mheshimiwa Dkt. Kalemani mdogo wangu, Naibu wake Mheshimiwa Subira Mgalu, Katibu Mkuu, Ndugu Mwinyimvua na watumishi wote wa Wizara ya Nishati, hongera sana kwa kazi nzuri mnayoifanya na napenda nianze kwa kuunga mkono hoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, dunia sasa inapima uwezo wa uchumi wa nchi kwa kuangalia uwezo wake wa kuzalisha na kutumia umeme. Kwa hiyo, ukitaka kupata kipimo kizuri cha kujua nguvu ya uchumi wa Taifa fulani, unaangalia wana uwezo gani wa kuzalisha nishati na wana uwezo gani wa ku-consume nishati hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe takwimu, nchi ya kwanza kwa kuzalisha umeme yaani energy per capital ni Iceland, nchi ya 73 ni China, nchi ya 137 ni Tanzania, nchi ya mwisho ni Eritrea. Katika grouping walizozifanya kwa clusters sisi ni wa 137 na uwezo wetu wa kuzalisha umeme ni megawatt 1,500. Ukiangalia kwa kiwango hiki utaona kwamba tunapozungumzia kupeleka umeme vijiji vyote zaidi ya 12,000, tunapozungumzia uchumi wa viwanda na kwamba mpaka mwaka 2020 tufike uchumi wa kati ni ndoto kama hatuna energy ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha wakati Serikali inafanya juhudi kubwa sana ya kuzalisha umeme na sera ya dunia ya nishati, The World Energy Policy is power mixing. Lazima uwe na vyanzo vya aina zote ili hiki kikitetereka unakitumia hiki, hiki kikitetereka unakitumia hiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwelekeo huu tunaokwenda wa kwenda uchumi wa viwanda ambapo pande zote mbili za Bunge tunakubaliana, hatuwezi kufika huko kama bado suala la uzalishaji wa umeme kwa nchi yetu siyo suala la kufa na kupona. Ni lazima liwe suala la kufa na kupona, ni lazima tuzalishe umeme wa aina yoyote ili tuweze ku-fit kwenye hicho tunachokitaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi siyo Mchumi na wakati mwingine napenda kusikiliza hotuba ili nijifunze kwa sababu kujifunza hakuna mwisho. Inanisumbua napoona hata wabobezi wa uchumi waliopo humu wana-undermine jitihada hizi zinazofanyika. Sababu zenyewe zinazotolewa, nimesikiliza sana wasemaji wengi wanasema tuache Stiegler’s Gorge, tusizalishe umeme huu mradi ulioanza kufanyiwa study mwaka 1972 mpaka leo haujatekelezwa, tuachane nao na sababu wanazozitoa ni kwamba kwa kuwa tuna gesi hatuna haja ya kuzalisha umeme huu kwa sababu gesi tunayo tuzalishe umeme wa gesi. Wakati wanajua kabisa kwa sasa hivi the leading generation katika nchi ya energy ni gesi ambayo ina megawatt zaidi ya mia saba na arobaini na kitu, inayofuatia ni hydro ambayo ina mia nne themanini na kitu karibu 500, zinazofuatia ni ndiyo biomass na vitu vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa sisi suala la kuzalisha umeme wa hydro ni la kufa na kupona. Miradi mingi ya hydro duniani huwa inapata upinzani mkubwa na hupata upinzani mkubwa kwa sababu tu umeme wake ni wa bei rahisi na unaweza ukaiibua nchi hiyo kutoka kwenye umaskini na kuwa nchi yenye uchumi stable. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Waganda wanajenga Bujagali upinzani ulikuwa mkubwa, wakasema tunajenga kwa pesa zetu na wakajenga kwa pesa zao. Vyanzo vya maji yanayozalisha umeme ule wa Bujagali, Kabahale ni vyanzo vya Mto Nile ambapo kuna siasa nyingi na international affairs nyingi lakini bado wame-generate umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, installed capacity ya Ethiopia ni megawatt zaidi ya 4,000 na wamezi-tap kwenye Mto Nile wakajenga mradi, unazalisha umeme na walikataa kusaidiwa na mtu yeyote wakaamua kuzalisha kwa pesa yao. Hivi sasa Ethiopia wana mradi unaoitwa The Grand Ethiopian Renaissance Dam ambao utazalisha megawatt 6,450 na wanachukua Mto Nile. Sisi tunazuiwa na Watanzania wenzetu wanaosema ni wazalendo, kukata miti square kilometer 1,400. (Makofi)

TAARIFA . . .

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: Mheshimiwa Mwenyekiti, mzungumzaji ni mdogo wangu na nampenda sana rafiki yangu, alipokuwa anagombea Urais Chuo Kikuu nilimsaidia pia. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania tunapaswa kulichukua jambo hili kwamba siyo la kisiasa, ni jambo letu sote na ushindi wa kujengwa kwa chanzo hiki cha umeme iwe ni wa kwetu sote. Ili tuweze kufika kwenye uchumi wa viwanda, kwanza ili tuweze kupeleka umeme kwenye vijiji vyetu vyote zaidi ya 12,000 tunahitaji zaidi ya megawatt 2,500 ambazo hatuna. Sasa anayesema anataka umeme wa REA kijijini kwake ndiyo huyo anayekataa chanzo chenye bei nafuu kuzalisha umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania katika ukanda huu wa East Africa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)