Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Nishati

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Nishati

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi. Kwanza nianze kuunga mkono hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati. Naomba niende moja kwa moja kwenye jambo ambalo lina manufaa makubwa kwa nchi yetu lakini baadhi ya wachangiaji wamekuwa kidogo wanapotosha wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiangalia miundombinu, tukianza na reli, mkoloni alivyojenga reli kuanzia Dar es Salaam mpaka Kigoma na Mwanza alisafisha miti na walivyojenga barabara walisafisha miti. Kwa hiyo, unavyotengeneza miundombinu yoyote kwa manufaa ya wananchi lazima utagusa mazingira. Kwa misingi hiyo, ujenzi wa Bwawa la Stiegler’s Gorge linagusa mazingira lakini kwa asilimia tatu ya eneo lote la Selous. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia kwenda kwenye nchi ya viwanda kama wenzangu ambavyo wameweza kuzungumza, lazima tuwe na umeme wa uhakika na vyanzo mbadala ambavyo ni zaidi ya kimoja. Nitaomba nijikite kidogo kwenye faida za kuwa na hili bwawa. Jambo la kwanza, Wabunge wengi wamezungumzia kuhusu TANESCO kufanya biashara kwa hasara, lakini hawajajiuliza kwa nini imefanya kwa hasara. Kwanza, ni nafuu ambayo imewekwa kwa wananchi kwa bei ambayo haiendani na soko na gharama za uzalishaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kitabu cha Waziri ukiangalia upande wa kuzalisha unit za umeme kwa kutumia maji ndiyo wenye bei nafuu, kwa shilingi za Kitanzania 36 kwa unit, kwa dola ni dola 1.63. Katika umeme tunaoutumia kwa sasa hivi wa megawatt 1,517 ni asilimia 37 tu inatokana na maji. Kwa hiyo, niombe Serikali huu mpango tunauunga mkono endeleeni, msiangalie nini watu wanasema, angalieni matakwa ambayo yalianzishwa na Baba wa Taifa tangu mwaka 1972. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna faida ya ajira, maji hayo pia yatatumika kwa ajili ya matumizi ya majumbani. Wananchi na Wabunge wengi wa Mtwara na Lindi walikuwa wanazungumzia kutoa maji kutoka Mto Rufiji kupeleka Mtwara na Lindi, hii itakuwa ni suluhisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakuwa na uvuvi na sasa hivi tuna teknolojia ya kuwa na zile cage za uvuvi. Ziwa Victoria ipo, watu wanaotoka Musoma na Mwanza wanajua na wavuvi hapa wapo, itakuwepo. Tutakuwa na utalii, katika ujenzi watu wanaenda China wanatembea kwenye ule mlima wanaangalia lakini hapa pia tutakuwa na utalii wa ndani na nje tutaweza kuvutia na tutaongeza mapato ya ndani na GDP yetu itapanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.