Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami naomba nichukue fursa hii kuwapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na timu yake nzima ya wataalam kwa kazi wanayoifanya.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ulikuwa ni mmoja, kama inawezekana, Serikali ikae tuangalie mfumo wa kubadilisha. Leo hii tunapanga matumizi kwanza halafu ndiyo tunaenda kuyatafutia mapato. Nashauri kwamba tuangalie namna kwamba tukusanye kwanza halafu ndiyo tuyapangie matumizi. Haya yote tungeondokana nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia tubadilishe budget circle, kwa mfano, badala ya sisi huu muda Wizara zote, taasisi zote, kila mmoja ameshapanga bajeti yake, kuleta mabadiliko hapa ni ngumu, yaani utafanya mabadiliko labda kwa asilimia moja au mbili. Tungekuwa tunakaa mwezi wa nane mpaka wa kumi na mbili ili mambo yote ambayo tunataka kushauri tuweze kushauri ili yaweze kuingia kwenye circle kama kodi za kupanda, kuna vitu vya kuondoa, nini kiongezwe ili wanaopanga bajeti zao wajue kabisa hii nikipanga inakubalika na kutokana na mapato ya uhakika ambayo tunatarajia, tutaweza kwenda vizuri.

Mheshimiwa Spika, la pili naomba Wizara ya Fedha, kwa sababu mapato na matumizi yote nyie ndio mnaya- control. Ni vizuri mngejitahidi kuangalia mifumo hii yote ya kulipa iliyopo, muangalie namna yaku-integrate yaani hizi mifumo yote iwe imeunganishwa ili kama Wizara ya Fedha, kwa mfano kuna dai lolote linaanza ngazi ya Halmashauri au kwenye Taasisi yoyote, nyie mnaiona moja kwa moja. Mpaka ifike hatua ya kuwafikia ninyi, kama kuna maswali mnakuwa tayari mmeshauliza.

Mheshimiwa Spika, vile vile iunganishwe na Ofisi ya CAG ili muda wa uhakiki uondoke na mambo yaende kwa haraka zaidi. Tukiwa vizuri na mifumo hiyo, nina uhakika kwamba masuala haya ya uhakiki na nini hayatakuwepo. Pia ni vizuri sasa tuendelee kuangalia namna ya kuboresha Chuo chetu cha Kodi ili iweze kufanya shughuli yake vizuri zaidi na elimu itolewe kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, pia kwenye suala la utafiti na maendeleo, ni vizuri tuwekeze zaidi kwenye utafiti ili kujua mifumo mbalimbali wapi tunaweza tukawekeza Serikali ikafanya vizuri na tukapata kodi nyingi zaidi na tuweze kuangalia mifumo mbalimbali. Kwa nini sekta isiyokuwa rasmi inazidi kukua na sekta rasmi inazidi kupungua. Ni vizuri tukiwekeza zaidi kwenye masuala ya utafiti. Haya yote yanawezwa kufanywa tukiwa na Tume nzuri na Tume ya Mipango ambayo itaweza kuratibu mambo yote hayo ili tuweze kupata maendeleo.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine la kuangalia, kwa sababu yote hii iko chini ya Wizara ya Fedha, taasisi zote ambazo zinatoa elimu kwenye masuala ya kodi, masuala ya uhasibu, masuala ya clearing and forwarding, mara nyingi ukikuta wataalam wa uhasibu wakifanya makosa au wale wa clearing and forwarding anayeumia ni yule mteja.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wakifanya makosa kwenye ethics, unakuta anayeumia ni mteja. Sasa hiyo inaleta changamoto kwa wateja kwani gharama zinapanda, zinakuwa juu.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo ni muhimu ni suala lile la kuleta blueprint, kwa sababu Wizara ya Fedha ime-base zaidi kwenye makusanyo na tusipopata ile blueprint mapema bado tutakuja kuambiwa huko mbele kwamba tumeweka chini ya mwamvuli mmoja, lakini bado tozo na ada ambazo ni kero kwa biashara zetu zitaendelea kuwepo. Kwa hiyo, uzalishaji wa bidhaa mbalimbali za viwanda hapa nchini gharama yake itakuwa ni kubwa na tutashindwa kushindana na bidhaa ambazo zinatoka nje ya nchi.

Kwa hiyo, kabla ya kufikia huko kwenye bajeti kuu ni vizuri jukumu hilo, Wizara ya Fedha iunganishe Wizara nyingine zote na Taasisi ambazo ziko chini yake, kama Serikali basi ije ituletee mapema ili tuweze kuifanyia kazi mapema.

Mheshimiwa Spika, mwisho pia kwenye suala zima hili la procurement, ni vizuri kwamba Serikali kwa kupitia Wizara ya Fedha muweze kuangalia kwamba hizi Taasisi zetu je zinafanya vizuri? Kwa mfano, PPRA na GIPSA ili tuweze kuleta mafanikio.

Mheshimiwa Spika, ahsante, naunga mkono hoja.