Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, naomba kuzungumzia kuhusu bajeti ya own source asilimia 40 maendeleo badala ya asilimia 60 ya awali. Halmashauri ya Mji wa Geita ilitenga asilimia 60 ya mapato ya ndani (own source) kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Hivi karibuni Wizara yako imetoa maelekezo kwa Halmashauri yangu ya Geita Mjini kubadilisha mipango kutoka asilimia 60 ya own source kwenye maendeleo kwenda asilimia 40 na hivyo kufanya matumizi ya kawaida kuwa makubwa kuliko miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri yangu haioni sababu ya kubadili mipango yote ya bajeti ya fedha ambazo sisi wenyewe tumekusanya kwenye vyanzo vyetu wenyewe na tumekaa, tumeona tuzielekeze kwenye miradi ya maendeleo ambayo ndiyo vipaumbele vyetu. Naomba kupata ufafanuzi kuhusu sababu ya Wizara hii kutoa mwongozo ambao unaondoa vipaumbele vya maendeleo kwa matumizi ya kawaida.

Mheshimiwa Spika, lingine ni madeni ya wazabuni mbalimbali. Pamoja na jitihada kubwa ya Serikali kulipa madeni, bado Wizara ya Fedha imeshindwa kuwalipa wazabuni wanaoidai Serikali kama wazabuni wa shule, magereza na taasisi za umma. Wazabuni wa pembejeo wanadaiwa na benki. Naomba juhudi za Serikali kupitia upya madeni hayo zifanyike mapema na kuleta orodha ya wauzaji wenye tuhuma za kuwapeleka mahakamani na kuwashitaki ili vyombo vya haki viweze kuona ni nani anastahili na nani hastahili kulipwa.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu PRIDE kushindwa kulipa fedha za wateja na mishahara. Yapo malalamiko makubwa kuhusu PRIDE Tanzania. Ipo taarifa kwamba wafanyakazi wana miezi 18 bila kupata mishahara na wateja walioweka akiba ya fedha wamekosa huduma kwa kuwa fedha hakuna.

Mheshimiwa Spika, zipo taarifa kwamba management ya juu ya PRIDE imekimbia na zaidi ya shilingi bilioni 40 za fedha hii, kuna sehemu ni mali ya umma. Naitaka Wizara kutoa tamko kuhusu ukweli wa hali ilivyo PRIDE Tanzania na hatua zinazochukuliwa kulipa madeni ya wafanyakazi na wananchi walioweka akiba zao.