Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia moa moja. Nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Makatibu Wakuu na watendaji wote wa Serikali kwa kazi kubwa wanayoifanya. Ninao mchango wangu katika mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, naishukuru sana Serikali kwa kutoa fedha za miradi ya kimkakati katika Halmashauri zetu. Ni jambo jema sana na nina hakika kile kilio chetu cha kudai kodi zetu za majengo kimepata majibu. Nashukuru sana Serikali naomba tuendelee hivyo, watukusanye fedha wazirudishe kwenye miradi ya kimkakati.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali isaidie Halmashauri ya Temeke kulichukua deni la CRDB Bank ambazo Manispaa ya Temeke walikopa kwa kulipa fidia katika mradi wa DMDP lakini Halmashauri nyingine walipewa fedha hizo na Serikali. Deni lile ni kubwa na lina riba na chanzo kikubwa kilichoshawishi Halmashauri wachukue ni kodi za majengo ambazo hazipo kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, naomba sana Serikali isaidie Halmashauri, vinginevyo tunajisikia vibaya na tutakosa miradi ya kasi kuwa wa kwanza katika kutekeleza maagizo ya Serikali. Serikali wakae na Halmashauri zetu kuangalia biashara gani zinazopaswa kulipiwa kodi na zile ambazo hazitakiwi kulipiwa kodi wananchi waelewe. Kuna biashara zinatozwa kodi lakini ukiangalia mtaji wake ni wa shilingi 500,000 tu. Serikali ina taasisi nyingi za fedha za kusaidia wananchi kupata mikopo na fursa mbalimbali kama UTT na kadhalika. Lakini wananchi hawazitambui, Serikali ifanye juhudi za makusudi kuzifanyia mkakati wa kuziweka wazi kwa wananchi zinaweza kutusaidia kuondoa umasikini.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia hoja.