Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa sana naomba nimjulishe Mheshimiwa Waziri kwamba baba yangu Mzee Mohamed Said Bobali amestaafu utumishi wa umma tangu mwaka 2010 lakini hadi leo hii bado hajalipwa pensheni yake. Mzee huyu aliajiriwa na Idara ya Ujenzi na baadae akahamishiwa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, hivyo kahamishwa na Mfuko wake wa Pensheni tangu mwaka huo, Mfuko wa Pensheni wa Watumishi wa Serikali za Mitaa na Hazina wamekuwa wakishindana ni nani anapaswa kumlipa mafao yake? Jambo hili ni kinyume kabisa na haki za binadamu na haki za wafanyakazi kama zinavyoelezwa na ILO.

Mheshimiwa Waziri, naomba sana Wizara yako ifanye intervention juu ya jambo la mzee huyu kwani linamsababishia stress na manung’uniko sana. Si vyema Serikali ije ilipe mirathi ili hali mhusika aliwahi kustaafu salama, salmini.

Kuhusu tozo kubwa za kuingiza fedha kutoka nje ya nchi; Mheshimiwa Waziri Jumuiya ya Watanzania waishio nje ya nchi (diaspora) ni moja ya kundi muhimu sana katika uwekezaji humu nchini ikiwa Serikali itaweka taratibu rafiki za kuvutia kundi hili kuja kuwekeza nchini. Moja ya kikwazo kikubwa ambacho wamekuwa wakikisema ni tozo wanayotozwa wanapotaka kuingiza fedha nchini jambo linalopelekea wao kuanza kuwekeza nchi nyingine tofauti na Tanzania.

Mheshimiwa Waziri, kwa nini msiweke utaratibu mahsusi ili kuwavutia watu hawa kurudisha nyumbani mitaji yao kwa wao kuja kuwekeza hapa nchini. Hali ilivyo pia inachangia watu kuingiza fedha kwa njia zisizo halali hivyo kuikosesha Serikali mapato yake.