Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu kutoza kodi kabla ya kufungua biashara; TRA imekuwa ikikadiria kodi za wananchi wanaotaka kufungua biashara kabla ya kuanza biashara bila kujua kama biashara hiyo itaingiza fedha kiasi gani, matokeo yake wafanyakabishara wanaendesha biashara kwa hasara. Mfano, kuna Mbunge amefungua biashara yake baada ya kukadiriwa kiasi cha mtaji wake shilingi 3,000,000, wakamkadiria kulipa shilingi 22,000 kwa miezi mitatu, ambapo jumla yake kwa mwaka atalipa shilingi 834,000, hadi sasa Mbunge huyo kwa siku anaingiza shilingi 5,000 hadi shilingi 20,000. Maana yake anakusanya fedha zote kwa ajili ya TRA tu. Naomba Serikali ifuatilie TRA, ni kwa nini wanaanza kuwatoza wafanyabiashara kabla ya kuwapa muda wa matazamio ya biashara zao.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mashine za EFD; tatizo la EFD ni kubwa, hadi sasa kuna mfanyabiashara na hasa wanaoanza biashara wamelipia mashine za EFD shilingi 650,000 lakini hadi sasa hawajapata mashine hizo kwani wameambiwa mtandao uko chini. Hivyo, wametumia risiti za mikono ambapo wateja wanagoma kupokea risiti za mkono. Ninaomba Serikali ishughulikie suala hili haraka iwezekanavyo kwani Serikali yenyewe inapoteza mapato yake.

Mheshimiwa Spika, tukiwa hapa Bungeni Serikali ilitamka hapa ndani Bungeni kwamba road license imefutwa badala yake fedha imeingizwa kwenye mafuta. Kuna wananchi ambao hadi sasa magari yao yameshikiliwa na TRA. Mfano, kuna mwananchi mmoja pale Njombe ambapo gari yake inaendelea kushikiliwa pale TRA kwa kudaiwa road license ya huko nyuma. Naomba Serikali ifuatilie suala hili na kuona kwamba magari hayo yanaachiwa.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.