Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, nianze na suala la upelekaji fedha Wizarani kwa ajili ya miradi. Kutotoa pesa za mradi kwa wakati ni changamoto kubwa sana kwa asilimia tano kwenye miradi mbalimbali na kupelekea kuzorotesha miradi ya maendeleo. Nikichukulia Wizara ya Mambo ya Ndani kazi nyingi zimeishia njiani na kupelekea kupoteza fedha nyingi zilizokwishatumika katika miradi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu fedha shilingi trilioni 1.5; mnamo mwaka huu kulitoka report ya mkanganyiko ya mwaka 2016/2017 kuna hoja ya shilingi bilioni 203.9 ya Serikali Kuu ya Tanzania kwamba ulikusanya kwa niaba ya SMZ, hii si kweli kwani SMZ mwaka 2016/2017 bajeti yao ilikuwa shilingi bilioni 841 na kati ya hizo shilingi bilioni 452 ni vyanzo vya ndani na nje na shilingi bilioni 58.9 katika mapato ya ndani, mapato ya kodi yalikuwa shilingi bilioni 366.0; makusanyo ya ZRB na TRA na mapato yasiyo ya kodi shilingi bilioni 23.6. Shilingi trilioni 1.5 ni karibu mara mbili ya bajeti yote ya Zanzibar. Naomba kujua zipo wapi?

Mheshimiwa Spika, Wizara imeonesha udhaifu kusimamia Deni la Taifa kwa kuwa deni limezidi kuongezeka na kuwa na athari za kitaifa; mid-year review katika mwaka 2017/2018 iliyotoka mwaka huu Februari, 2018 ni kwamba Deni la Taifa liliongezeka kwa dola 1,054.6, sawa na shilingi trilioni mbili, bilioni mia tatu na milioni mia moja ishirini. Deni limefikia trilioni hamsini na tisa, bilioni thelathini na saba. Ni shida kwa Taifa.