Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Spika, Ofisi ya TRA Njombe Mjini ni finyu sana kiasi kwamba inasababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi ambao wanafika TRA katika kuhitaji huduma mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, suala la kodi ni suala muhimu sana na wananchi wa Njombe wamelipokea vizuri kwa kitendo cha mwananchi kushinda TRA ili alipe kodi hii imewavunja moyo sana walipa kodi. Ninachohitaji kufahamu ni lini Serikali itajenga jengo lenye nafasi ya kutosheleza mahitaji ya TRA- Njombe kwa kujenga jengo la kutosha Njombe, hiyo itasaidia sana kurahisisha kazi ya kukusanya mapato ya Serikali. Watumishi wa TRA ni wachache sana, ni lini Serikali itaongeza watumishi TRA Njombe?

Mheshimiwa Spika, mbao laini ni zao la kawaida kwa Njombe, wakivuna miti yao wanadaiwa risiti ya EFD. Nahitaji kufahamu kwa nini wakulima hawa wa miti wanapokuwa wanasafirisha mazao yao ambayo ni mbao wanadaiwa EFD receipt? Je, wakulima wa korosho nao wanatakiwa kuwa na EFD receipt au wakulima wa miti wanaonewa? Ni lini sasa Serikali itaweka ufafanuzi wa namna gani wakulima wa miti wanaweza kusafirisha mazao yao ya mbao?

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.