Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Spika, napenda kuunga mkono kwa mchango ufuatao:-

Mheshimiwa Spika, fedha za miradi haitoki, hivi karibuni Serikali iliitisha mkutano wa Wenyeviti wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Wakurugenzi na Maafisa Mipango kuainisha miradi michache ambayo itakuwa muhimu kutoa fedha, iliorodheshwa lakini mpaka sasa hakuna fedha iliyotolewa na Serikali. Mara kadhaa inasema fedha ipo, naomba ipelekwe kwenye miradi hii.

Mheshimiwa Spika, tuliwatangazia wananchi kuwa sasa Serikali yao imewakumbuka, pelekeni fedha ya miradi kwenye Halmashauri ambako miradi ya afya, miradi ya vituo vya afya, miradi ya zahanati, miradi ya maji vijijini, miradi hii imeathirika vibaya.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha haitoi fedha zinazoidhinishwa na Bunge kwenye miradi mingi ikiwemo ya maji, ile miradi ya vijiji kumi na REA pia imeathirika sana. Wizara ya Fedha isijichanganye, mwaka jana tuliambiwa mkulima atasafirisha mazao gunia kumi nchi nzima, Halmashauri wanadai, wafanyabiashara wadogo wanaosafirisha mazao tani moja na walitoa barua ya ufafanuzi ikidai mkulima pekee ndiyo inamhusu, tena siyo mchuuzi mdogo mdogo, ipi ni ipi tuelezeni tuelewe.

Mheshimiwa Spika, mikopo kwenye mabenki imebana sana, trend ya uchumi kwenye mabenki yote yanapiga kelele kudorora na mikopo midogo midogo haipatikani. Tunaomba masharti yapozwe kidogo ili wananchi waione fedha kwenye mzunguko wa kila siku. Wizara itoe fedha ya kununulia mazao ya wananchi ili wakulima wapate maendeleo na viwanda vipate kuanzishwa kwa vile malighafi itaweza kupatikana. Wizara ya Fedha ilipe madeni ya Mawakala wa Pembejeo.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha itoe kipaumbele kwenye utoaji wa fedha za kibajeti zote. Hatuwezi kukaa Bungeni kupanga bajeti za Wizara unafika mwisho wa mwaka unakuta Wizara imetoa fedha wakati mwingine chini ya asilimia 20 ya bajeti, kwa nini?

Mheshimiwa Spika, nataka kuona fedha za Wizara zote ikiwemo ya Kilimo, Maji, Nishati, Afya na kadhalika, kulingana na matamko ya kitaifa na mikataba tulioridhia. Malipo ya makinikia, malipo ya watumishi mbalimbali kama walimu.