Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

Hon. Mariamu Ditopile Mzuzuri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Awali ya yote napenda kusema kwamba naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Simbachawene kwa asilimia mia moja. Pia nampongeza Mheshimiwa Rais, kwa kweli amekuwa kwa hakika akiwa ni mtekelezaji mzuri wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa kulifanya Dodoma kuwa Jiji, tuna uhakika sasa kweli Makao Makuu ya nchi yapo Mkoa wa Dodoma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, narejea tena kumpongeza Mheshimiwa Rais na nimwambie, mimi kama mwakilishi wa vijana kutoka Mkoa wa Dodoma ambao sisi ndio tupo zaidi ya asilimia 60 ya population kwamba hilo tumelipokea na kwa kweli tutapokea changamoto zote na Dodoma kweli litakuwa Jiji. Niseme tu, kwa hili kumrudishia, tunajua mtanange 2020 upo, atashinda kwa asilimia kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna nchi za wenzetu hapa Afrika zimeweza. Mfano Nigeria na ya pili, South Africa. Kama wao wameweza na sisi tutaweza. Kwa hiyo, kama kuna mtu yeyote ambaye hajaunga mkono hoja hii, ajue kwamba sisi tumeweza na tutaweza. Kwa hiyo, la msingi tu apande pamoja na sisi tushirikiane kwa ajili ya kuhamisha Makao yetu Makuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, Mheshimiwa Rais alisema Morogoro kwamba katikati pazuri. Dodoma tumelala katikati ya nchi ya Tanzania na tunaona barabara imejengwa chini ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi, kuunganisha Iringa, Arusha na nchi ambazo zipo Kanda ya Ziwa. (Makofi)

Kwa hiyo, kuweka Makao Makuu hapa katikati kutarahisisha hata uchumi wa ujenzi wa viwanda na huduma zote. Mtu kutoka Arusha ili apate huduma za Kiserikali hawezi kuzunguka kwenda mpaka Dar es Salaam. Mtu kutoka Iringa, Mbeya ni rahisi kufika Dodoma kupata huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme jamani, katikati pazuri. Kweli Mheshimiwa Rais tunamshukuru, naunga mkono hoja.