Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

Hon. Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA ZA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kuunga mkono hoja iliyotolewa hapa Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, nawaomba sana Waheshimiwa Wabunge wenzangu, katika watu wanatuishi kwa upendo mkubwa sana sisi Waheshimiwa Wabunge ni ndugu zetu wa Dodoma. Kauli zetu zisiwafadhaishe wenyeji wa Dodoma. Hili ni jambo la kwanza, lazima tuliweke sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wWakati Mheshimiwa Rais anakusudia hili jambo jema ambalo lina maslahi mapana kwa nchi yetu, halafu na sisi viongozi tuliopewa dhamana tukionekana tunatoa mishipa kama vile jambo hili siyo jema, nadhani tunawanyong’onyeza sana kwa kiwango kikubwa wenyeji wetu wa Dodoma, hili ni moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, ni kwa sababu Azimio hili lilikuwa ni suala zima la maelekezo ya kisheria ije Dodoma. Niseme kwamba Ofisi yangu ipo katika maandalizi ya mwisho kabisa ya hii sheria ya kuja Dodoma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine katika suala la miundombinu, Ofisi yangu ambayo ina mamlaka ya kufanya hivyo, mwaka huu hapa Dodoma tumetenga zaidi ya shilingi bilioni 35 kwa ajili ya ujenzi wa soko la kisasa, stand ya kisasa pamoja na recreation area. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kupitia TARURA lengo letu ni kwamba tunataka tutengeneze barabara za pete za kutosha, nanyi sasa mnafahamu, hata ukitoka St. Gasper unakuta barabara nyingine zimefunguka. Lengo letu ni kwamba tuwe na ring road za kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaambie ndugu zangu, Dodoma ndiyo itakuwa ndiyo Mji wa kwanza the best hapa Tanzania kwa upangaji mzuri. Ofisi yangu imeelekeza na hivi sasa tumekamilisha viwanja 15,000 eneo la Mtumba vimekamilika na hivi sasa watu wapo foleni kugombania hivyo viwanja kwa ajili ya mustakabali wa Dodoma. Kuna viwanja 21,000 tunavipima maeneo ya Ihumwa kule. Lengo letu ni kwamba tuhakikishe Mji wa Dodoma ndiyo Mji mzuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge, mnafahamu, hata ukiwa unashuka na ndege, ukiwa unashuka Dodoma ni tofauti kama unaposhuka maeneo ya miji mingine. Hili ni jambo la kujivunia kwetu sote. Kubwa zaidi katika hili, najua Mheshimiwa Rais amepewa kwa mujibu wa Sheria Sura Na. 288 katika kifungu cha (5)(3) katika suala zima la uanzishaji miji, tukipitia sheria tutajua haya mambo ni jinsi gani Mheshimiwa Rais hakukurupuka alifanya kwa mujibu wa Sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, halikadhalika kwa sababu Mheshimiwa Rais amepewa dhamana na Watanzania na dhamana aliyopewa kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Ilani imeainisha jinsi gani Serikali hii itahamia Dodoma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika agenda ya comparison, nadhani kuna kitu kidogo kilikuwa na sintofahamu kuona kwamba Mheshimiwa Rais kwa nini aliwabagua watu wa Moshi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaambie ndugu zangu, Moshi kilomita za mraba ni 58 peke yake. Naomba niwaambie, tukienda katika utaratibu wa vigezo, Wabunge wa kule wanafahamu. Ndiyo maana kulikuwa na suala zima la extension hata kuhakikisha kwamba kuna vikao vingine watu Hai watenge maeneo yao kwa ajili ya jiji la Moshi. (Makofi)

Kwa hiyo, mambo haya yalikuwa katika mchakato zaidi. Kama Moshi yenyewe, kilomita za mraba pale ni 58, naomba tuelezane ukweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ngoja kwanza, nawaeleza fact, kwa nini kila jambo linaenda kwa mujibu wa sheria? Ukianzia hilo sasa, ndiyo maana hata Moshi yenyewe naomba niwaambie, wewe Mhehimiwa Komu, subiri… (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais jambo lolote anashauriwa kwa wema. Naomba niwaambie, hakuna jambo lolote unaweza ukashauri kwa hasira. Kila kitu busara inatawala kufanya mambo yaweze kukamilika.