Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nimepiga kelele sana humu ndani, nachangia kwa nguvu mno lakini mambo ni yale yale mpaka koo limeharibika sasa, leo nitachangia taratibu sitapiga kelele sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye taarifa ya Mheshimiwa ndugu yangu Mheshimiwa Dkt. Mipango, ukurasa wa 81 alikuwa anamlinganisha Mheshimiwa Magufuli na watu maarufu waliofanya mambo makubwa duniani. Sasa na mimi nimeingia kwenye Google hapa nikajaribu kuangalia, amemtaja mtu anaitwa Park Chung Hee, huyu amezaliwa mwaka 1917 na amekufa mwaka 1979 lakini alikuwa assassinated maana yake aliuwawa. Alikuwa mwanajeshi tangu mwaka 1944 mpaka 1945 na alikuwa cheo cha Jenerali halafu alikuwa ni Dikteta. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mtoto wake pia wa kwanza alikuja akawa mwanamke wa kwanza kuwa Rais wa Korea. Kwenye historia inaonyesha tarehe 10 Machi, 2017 aliondolewa madarakani kwa kupinduliwa kwa tuhuma za rushwa. Historia inaonesha pia tarehe 6 Aprili, 2018, huyu mwana mama aliyekuwa Rais wa Korea (South Korea) amefungwa jela miaka 24 kwa tuhuma za rushwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nilipoangalia historia hii nikasema haya maneno inabidi Mheshimiwa Dkt. Mpango ayafute kwa sababu Mheshimiwa Rais wetu hafanani na mambo ya namna hii. Afute maneno haya sio sawasawa. Nadhani Mheshimiwa Dkt. Mpango atakuwa labda ame-quote vibaya lakini hii uindoe historia imekaa vibaya, nilikuwa nataka nianze hapo. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitatumia kitabu cha Mheshimiwa Mpango, ukiacha hilo andishi moja tu ambalo nimeona lina shida, ameandika maneno mazuri kwa sababu amekiri vizuri na nitapitia maeneo machache aliyosema ukweli. Nampongeza sana Mheshimiwa Mpango kwa kusema ukweli.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mpango yeye ni msomi mchumi, mimi ni mwalimu sielewi, ni mwanasayansi tu wa kawaida lakini 2016 uchumi ulikua kwa asilimia 7, mwaka 2017 ulikua kwa asilimia 7.1, mwaka2018 ulikua kwa asilimia 7.2. Mimi naomba Mheshimiwa Dkt. Mpango atusaidie hivi ukimueleza mtu wa kawaida yaani miezi hii kwa mwaka huu kwamba uchumi umekua ataelewa yaani Mbunge wake sielewi, atusaidie Watanzania waelewe, yaani hii ina-reflect vipi maisha ya kawaida ya wananchi? Kwa kweli hii napata nayo shida sana, unaweza ukaeleza hapa na fomula umeandika, wananchi wa kawaida wanataka kuona kama unasema uchumi unakua, mzunguko wa fedha mtaani uwe mkubwa uonekane, bidhaa ipatikane, watu wapate mahitaji ya kawaida. Sasa hiyo lugha hapa mimi siioni kwa kweli unisaidie Mheshimiwa Dkt. Mpango kwa utalaam wako.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Bajeti ya Serikali 2016/2017 zilitengwa shilingi trilioni 29.5 hazikufika asilimia 80 katika utekelezaji wake. Mwaka 2017/2018 tulipitisha bajeti ya shilingi trilioni 31.7 sasa hivi taarifa inaonyesha ni asilimia 69 labda imeongezeka kabla ripoti haijaandaliwa. Hii bajeti ya sasa hivi ni shilingi trilioni 32.5, naomba unisaidie ni kwa nini tusiende na bajeti halisi? Tumeshatenga bajeti miaka kadhaa iliyopita tumeona fedha yetu ya ndani ni kiasi gani, tumeona misaada ikoje na mingine inakwama halafu tuseme hapa sisi uwezo wetu ni shilingi trilioni 20, tupange mipango ya shilingi trilioni 20. Hapa ndipo malalamiko yanapokuja kwamba tunawapa watu matumaini makubwa, bajeti kubwa, mambo mengi lakini hayafanyiki, inaonekana tunadanganya, nadhani hili pia lifanyiwe kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lingine ni kwenye ukurasa wa 14, Mheshimiwa Mpango amesema kiwango kikubwa cha umaskini kimekuwepo kwa Watanzania, ni maneno kwenye kitabu hiki cha hotuba. Anasema ukosefu wa ajira, sasa naomba unisaidie kwa hapa Mheshimiwa Dkt. Mpango. Maduka mengi yamefungwa huo ndio ukweli, watu wamefungwa biashara zao. Kama biashara zinafungwa maana yake mzunguko wa fedha unapungua, wananchi wa kawaida wale ambao waliokuwa wamepata ajira hawana ajira tena, uchumi unakuwaje hapa? Kwa hiyo, katika hili pia mliangalie.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna usafi wa kila Jumamosi, nimeona tu mahesabu ya kawaida, Watanzania wanaambiwa wafunge biashara zao kila Jumamosi asubuhi wanafungua saa nne haijalishi kama kuna famasi, kuna wagonjwa lakini wale mama lishe ambao wanapika chapati, wanaopika supu, huo ndiyo muda wa kupata hiyo huduma na hao wamejiajiri, sasa tunafanyaje hapa. Kwa hiyo, naomba mtuambie hii ratibu ya kila Jumamosi kufanya usafi tumepata faida kiasi gani na hasara kiasi gani ili tuweze kuamua maamuzi mengine tofauti na haya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine bar za Tanzania zinafunguliwa saa kumi zinafungwa saa tano usiku. Kule kuna Ma-barmaid walikopata ajira zao lakini kuna biashara zinafanyika wanalipa kodi. Kwa mfano, Dar es Salaam kuna foleni kweli kweli kama wewe umetoka mjini unafika nyumbani saa tatu, yaani unafika mtaani kwetu Kivule, Gongo la Mboto ni saa tatu usiku kwa mazingira ya Dar es Salaam, mwendo kasi haijafika. Maana yake hawa watakaa pale saa mawili wanazungumza bar inafugwa na ma- defender yanakamata watu kweli kweli, hawa watu wanalalamika. Kama kuna sheria ilikuwepo siku nyingi kwa nini isibadilishwe twende na wakati? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzetu Kenya hapa hao Usalama wa Taifa, Polisi wanatakiwa kuhangaika na watu ambao vipato vyao havijulikani wamepataje. Kama kuna mtu anakunywa, anakula, anavaa vizuri, ana magari mazuri hatujui kazi yake, hiyo ndiyo kazi ya Usalama wa Taifa kuwatafuta watu ambao wana vipato ambavyo havieleweki. Kenya hapo Nairobi huduma ni saa 24, biashara inazunguka, kila mtu anafanya kazi yake, watu wawajibike. Kwa hiyo, tusitengeneze mazingira ya kutisha watu, wafundishwe ustaarabu na wajitegemee na wafanye maamuzi sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukurasa wa 15 amezungumza habari ya kilimo, mifugo na uvuvi na amesema mwenyewe hizi sekta tatu zinawaajiri Watanzania asilimia 66. Sasa nimuulize Mheshimiwa Dkt. Mpango kwenye bajeti hii malalamiko yote ambayo Wabunge wamesema kwenye kilimo watu wamelima mazao ya pamba, tumshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu amechukua hatua lakini hata mahindi mpaka unaenda kwenye msimu mwingine haya mazao bado yapo mtaani. Mifugo imepigwa, imeteswa hakuna malisho, hakuna sehemu ya kuchungia, ugomvi na wakulima, Operesheni Sangara, leo mmezungumza habari ya samaki, haya mambo Mheshimiwa Mpango mngeyachukua mkakae pamoja mkayafanyia kazi mkatengeneza Taifa ambalo tunataka kwenda mbele badala ya kurudi nyuma tusirudie mambo yaleyale ya kila siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, iko hoja hapa Mheshimiwa Jenista ametoka nje, tulipokuwa tunajadili habari ya kuunganisha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii tulilalamika hapa kwamba ile formula iingizwe kwenye sheria. Waheshimiwa Wabunge ile formula haijaingizwa, sasa hivi kuna ugomvi mkubwa kati TUCTA na Serikali na wameshusha, ilikuwa 1/540 sasa imeenda 1/ 580. Mafao kwa mkupuo ilikuwa asilimia 50 kwa formula hii ambayo inalazimishwa wataalipwa asilimia 25,. Kwa mkupuo walikuwa wanalipwa asilimia 50 imeshuka zaidi ya nusu kwa yale mafao na kuna ugomvi mkubwa. Tulilalamika sheria iingizwe haijaingizwa wametunga kanuni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ina madhara kwa sababu hawa watumishi ambao, kwa mfano watu wa LAPF, PSPF wanaidai Serikali siyo chini ya shilingi bilioni 600 za madeni hayajalipwa na huu mzigo ni wa Serikali, hawa wastaafu wanachama wa vyama hivi ndiyo wataingia kwenye mzigo huu na hili ni janga la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama hauongezi mshahara Mheshimiwa Dkt. Mpango hawa wakienda kustaafu calculation ya mafao yao mwishoni inategemea increment ya kila mwezi. Ndiyo maana tunasema fuateni taratibu watu waongezwe pesa zao zitawasaidia siku za mbele katika maisha yao. Watu wanakufa haraka kwa sababu ya kukosa huduma nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nishauri jambo muhimu sana hapa, kwa mfano, kwenye Wizara ya Elimu ametaja data ndugu yangu Mheshimiwa Paresso sitaki kurudia yaani ukiangalia figure ya matundu ya vyoo, madarasa, nyumba za walimu, upungufu wa walimu, mimi nadhani Mheshimiwa Dkt. Mpango akija atuambie kwenye bajeti hii haya mambo yatatekelezwa kwa kiasi gani. Wabunge wamelalamika mmechukua kodi ya majengo, kodi ya mabango kwenye maeneo mbalimbali tumeathirika, haujarudisha asilimia Mheshimiwa Mpango, ungetuambia fedha hii imerudishwa kwa kiasi gani, haya mambo yangefanyika ingetusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nishauri jambo muhimu sana, kuna maneno mengi sana yanaendelea na kwa sababu mambo yanafanyika kwa haraka haraka sana kwa mazingira fulani hisia zinakuwa nyingi sana mtaani. Kwa mfano, mimi nimesoma ule Waraka wa Watumishi wa Mungu wa Waislam na Wakristu, mambo ambayo yametajwa, wanashauri hivi, tuwe na utawala bora, tufuate sheria, hii nchi haiongozwi kwa Ilani za vyama na matumizi mabaya ya dola. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, hivi haya mambo ya kutishiana, haya mambo ya kufuata utaratibu kuna kosa gani, Taifa hili humu ndani tumebaguana sana kivyama. Wabunge wa CCM, Wabunge wapinzani wakijadili wanadhani wengine wana haki zaidi kuliko wenzao kumbe Taifa ni la kwetu sisi wote. Tungeona tu kwamba hawa watu wanashauri, mimi nikitoa hoja ingepokelewa kwa nia njema kabisa kwa kujenga Taifa. Hii bajeti ni ya kwetu na ikipita siyo ya CCM ni bajeti ya Watanzania, iwe tumeunga mkono au hatujaunga, tusaidieni kupeleka Taifa mbele kwa kutuunganisha.