Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa asilimia mia moja. Naomba kutoa mchango wangu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Waziri unatambua kwamba Wizara yako iliahidi kushughulikia wizi uliofanywa na Karinzi Coffee Organic kwa kununua kahawa kwa wakulima 435 wa Jimbo la Kigoma Kaskazini na Manyovu 2014/2015 ambapo Serikali iliwaahidi kulipa malipo hayo ya dola za Kimarekani 75,000. Karinzi Coffee Organic inasema Kiwanda cha Kubangua Kahawa hawajawalipa. Tunakuomba kufuatilia suala hili kwani ni kero inayokatisha tamaa wakulima wa kahawa, tunakualika ufike Manyovu ukutane na wakulima wa kahawa kwani wewe utakuwa mkombozi wao.
Naomba ufuatilie juu ya kero ya pembejeo, muda wa pembejeo hizo kulingana na maeneo. Mkoa wa Kigoma unapokea mbolea nje ya muda ambapo tija yake haipatikani. Pili, wajibisha na tumbua majipu ya wezi wa pembejeo, Mawakala na Wakuu wa Wilaya.
Mwisho, nawatakia mafanikio mema.