Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AIDA J. KHENAN: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa dakika tano ni chache sana kuna mambo nategemea Waziri atakuja kutoa ufafanuzi ili tuweze kuelewa. Unapozungumzia kukua kwa uchumi leo katika kilimo wakulima wa mahindi ambao mwaka jana waliweza kuuza mahindi yao gunia Sh.60,000 leo ni Sh.24,000. Kwa hiyo, unapozungumzia kukua kwa uchumi mtuambie umekua sehemu gani.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo katika Taifa hili nimekaa nimefanya tafakari kubwa ni nani ana amani, mfanyakazi hana utulivu kwa sababu alitegemea sheria itamlinda kuongezeka kwa mshahara wake leo mshahara hauongezwi, mkulima hana amani kwenye Taifa hili, hali ya kilimo ni mbaya, njoo kwa wavuvi, njoo kwa wafanyabiashara, nani ana utulivu kwenye Taifa hili. Mheshimiwa Waziri wa Fedha wewe ndiyo unaweza kumshauri Rais vizuri kama unaweza kusikiliza mawazo ya Wabunge tunayozungumza humu ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo mfanyabiashara anajiona ni kama mkimbizi ndani ya Taifa lake. Ni kwa nini mmeshindwa kutengeneza mazingira rafiki kwa wafanyabiashara ni kutoza kodi zisizokuwa na sababu. Leo TRA wanajua hali ya uchumi ni mbaya lakini wakiamua kufunga wanafunga, huwezi kukamua maziwa ng’ombe usiyemlisha, unategemea wao wanapata wapi pesa. Taifa hili tunategemea wakulima, wavuvi, wafanyakazi, leo watu hawa wote wako kwenye wakati mgumu Taifa tunaliendeshaje? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sera ya kulinda uchumi wa Taifa. Tuliopo humu ndani siyo kwamba wote tumesoma uchumi tuko kwenye facult tofauti tofauti lakini ni pale ambapo unaweza kuchukua mawazo yetu ukaoanisha na taaluma yako kuweza kulipeleka Taifa mbele. Kama utachukua mawazo yako binafsi ndiyo haya tunarudi tena kuzungumza ndani ya Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vijana kama mimi wana wakati mgumu kwenye Taifa hili, ajira ni shida, wamejiingiza kwenye kilimo, kilimo hicho ndiyo imekuwa taabani hili Taifa tunalipeleka wapi? Waziri wa Fedha ukisema uchumi unakua wewe ndiyo unayempotosha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hali ni mbaya kuliko hiki unachokiandika, hii hali ni nzuri kwa nani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapozungumza mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara ni lazima tuangalie hawa wafanyabiashara wanapolipa kodi wanategemea wayaone matokeo ya kodi wanayoilipa. Leo hakuna matokeo yoyote ambayo yanaweza yakawaletea tija na wao kujisukuma kuweza kulipa kodi. Leo wanaona ukiwa mfanyabiashara ni bora ukae nyumbani. Hili suala ambalo tunazungumza kwamba mfanyabiashara ukimuelimisha akajua umuhimu wa kodi na akayaona matokeo hakuna ugomvi utakaotokea kwa sababu faida ya kulipa kodi anaiona. Leo mnatumia nguvu kuliko kutumia busara na maarifa inatuweka kwenye wakati mgumu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hili Taifa sio la Waziri wa Fedha ni Taifa la Watanzania, hiki unachokiandika unategemea kodi za Watanzania wakiwemo wakulima, wafanyakazi pamoja na wafanyabiashara. Ukijifungia mwenyewe ukaja na hizi takwimu unazozileta hapa zitaisha kwenye kitabu na haitakusaidia. Kwa sababu ulipoteuliwa na Rais aliamini ukija humu ndani utasikiliza mawazo ya Wabunge na sio mawazo yako. Haya mawazo tunayokwambia sisi kwamba unapozungumza hali ya uchumi umepima kwenye kipimo gani, ni kipimo gani ambacho umekitumia, wafanyakazi wanalia, wakulima wanalia, wafanyabiashara wanalia, wewe hizi takwimu unazipata wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Bunge pia tuna wakati mgumu na ndiyo maana tunasema Mheshimiwa Waziri wa Fedha zungumza ukweli. Ni lazima mbadilishe approach na Taifa lolote makini linakuwa na vipaumbele na kipaumbele sio cha kwako ni kipaumbele ambacho kinawagusa Watanzania na maisha halisi ya watanzania. Leo ukienda kwenye uhalisia hiki ulichokiandika haujaonesha mkakati wowote…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)