Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. RICHARD M. NDASSA: Naunga mkono, pongezi kwa Wizara kwa maandalizi ya hotuba. Naomba kutoa ushauri katika mazao ya biashara.
Zao la katani; leo hii pamba bei yake ilikuwa imedorora, tulikuwa tunaiita dhahabu nyeupe, katani leo White Gold. Miaka ya 70 katani katika soko la dunia, Tanzania tulikuwa tunaongoza, katani bora ilikuwa inatoka Tanzania. Soko la zao la katani limebadilika na kupanda bei ya katani (fibre), kwa tani ni dola 2,200 - 2,500. Serikali iangalie uwezekano wa kuliibua upya zao la katani.
Zao la pamba, nataka Serikali iwaambie wakulima wa pamba kuhusu mbegu zao (Kyuton) ambazo zimeua kabisa zao la pamba kutokana na wauzaji wa mbegu hizo zilizochakachuliwa kwa sababu ya rushwa. Leo naomba nipate maelezo ni nani hasa wamiliki wa kiwanda cha mbegu ziliozokuwa na manyoya. Hawa wameua kilimo cha pamba. Mbegu hizo zilipigiwa kampeni kubwa na viongozi kuanzia ngazi ya Taifa - Wizara na Wilaya, lakini tungependa kujua ni nani aliyewapeleka nje ya nchi Viongozi wa Juu wa Wilaya na Mkoa? Hii ni rushwa, sheria ishike mkondo wake kwa sababu kwa kufanya hivyo wamelizika zao la pamba kisa rushwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu usindikaji; Tume ya Mazao Mbalimbali tuliyozalisha; tuombe Serikali iangalie utaratibu wa kusindika na kuyaongezea mazao thamani. Mfano: mahindi, hakuna sababu ya kusafirisha mahindi, watumiaji wametaka unga siyo mahindi. Mpunga, watumiaji wanahitaji mchele na siyo mpunga, hapa naomba kwenye maeneo husika, kuwe na mashine za kusaga na kukoboa, lakini mazao haya yaani unga na mchele uwekwe kwenye mifuko ili kila mtu aweze kununua kufuatana na uwezo wake kilo 1, 2, 3 na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ng‟ombe, Watanzania wanataka nyama siyo ng‟ombe. Ng‟ombe wanakunya hovyo njiani, test ya nyama haipo. Kuku, Watanzania wanataka nyama ya kuku, unabeba kuku mzima na manyoya yake kwenda Dar es Salaam, kwa nini wasichinje hao kuku huko huko, nyama ikapelekwe kwenye supermarket na kadhalika.
Narudia tena, napenda na ningependa kujua ni hatua gani zilizochukuliwa kwa wale waliowatapeli wakulima wa pamba kwa kuwauzia mbegu za pamba zisizokuwa na manyoya zisizobeba, zilizosababisha kutoota vizuri tangu zilipotangazwa kwa mbwembwe sana na Viongozi wa Wizara yako. Ningependa kupata majibu yako.