Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze nami kuchangia mada iliyoko mezani. Kwanza ningependa kusema amani ni tunda la haki, mahali popote pale ambapo haki haitatendeka ni kwamba amani haiwezi kupatikana. Tutacheza, tutasema, tutachangia, tutafanya tufanyavyo lakini kama watendaji hawatatenda haki hakuna amani itakayopatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hayo kwa sababu kumekuwepo na kamata kamata, mauaji na hao wasiojulikana na vyovyote vile na wale wanaouawa mikononi mwa polisi. Hivi kama ungeweza kufikiria mtu anauawa mikononi mwa polisi, halafu useme kwamba kuna amani hao waliopata huo msiba wa kuuawa huyo ndugu yao mikononi mwa polisi wawachukulieje polisi hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema kabisa tutakaa tukafikiria hivi kama kweli tunataka kuzungumzia habari ya amani, tuangalie haki inatendeka kwa kiasi gani, ndipo tutaweza kusema kwamba sasa hivi Tanzania tuna amani ya kutosha kwa sababu haki inaenda sambamba na amani. Huwezi kupata amani kama hutendi haki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kama inataka kuhubiri amani tuone haki ikitendeka kwa watu wote na vyombo vyetu vya ulinzi vitende haki kwa wananchi ndipo tutasema kwamba Tanzania sasa hivi ina amani. Hatuwezi kusema theory wakati practical hazipo. Niishauri Serikali kama kweli Mheshimiwa Waziri wetu ana nia ya dhati ya kurejesha amani ile tuliyokulia sisi kwa umri huu, haki itendeke kwa wananchi wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshuhudia ubambikaji wa kesi, kijana anashikwa, kwanza utaratibu wa polisi kuwakamata wahalifu ni mbovu, kwa sababu sheria zinasema kabisa kwamba utamkamata, utamfikisha mahali akajieleze halafu kesi iende mahakamani, lakini mtu anampiga mhalifu, anageuka yeye kuwa ndio mahakama na kumsababishia maumivu na wakati mwingine kumsababishia kifo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sehemu zingine polisi wamempiga mpaka kijana mmoja anafika hospitalini anakufa, kwa sababu tu polisi hawajui kazi yao kwamba akishamshika mtuhumiwa huyo sio mhalifu tayari, mahakama ndio itakayosema kwamba yeye ana uhalifu na aingie jela. Hata hivyo, unakuta kwamba polisi anachukua hatua ya kumwadhibu wakati yeye siyo mahakama, tutasemaje kuna amani kama kuna mambo haya yanatendeka? Hiyo amani ambayo tunaihubiri ni ipi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuzungumzia upekuzi. Jamani hivi kweli unapoenda kumpekua mtu kuna sheria, tuna vitambulisho, unatakiwa kama ni kwenye mtaa kuna Serikali ya Mtaa, inatakiwa ishuhudie mtu anapekuliwa, lakini mtu anaingia yeye kama ni polisi anaanza pekupeku anaingia chooni, anaingia chumbani, anaingia huku, sehemu zote anaingia kwenye nyumba ya mtu. Hivi huyo mtu anajisikiaje, maana yake hata ile diginity yake inapotea. Kwa nini tufanyiwe hivi wananchi wa Tanzania, huko tulikotoka hatukushuhudia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina miaka yote hii sijawahi kuona Serikali ambayo inaruhusu mtu apekuliwe, ukiuliza unaambiwa nimeambiwa kutoka juu, huko juu ambako kupo juu sana, tunajua kabisa juu anakaa Mungu peke yake. Siku hizi anashusha directive kwamba sasa utafanya hivi na hivi ni kweli au huko juu anakoeleza kila siku ni wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda Mheshimiwa Waziri akija hapa atuambie huko juu wanakosema kila siku juu ni wapi huko tukakujue. Kama ni mbinguni tujue kitabu kinasema nini, Mungu alishusha biblia, alishusha maelekezo kwamba taratibu za kidini zitaenda hivyo. Huko juu sasa hivi ambako kila kitu juu, juu, ni wapi? Maana yake tumekuwa hatuelewi huko juu ni wapi? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ambacho ningependa kusema ni upepelezi wa kesi. Mahabusu anakaa miaka sita kwa sababu upelelezi haujatimia, huyo mahabusu akishakaa miaka sita aje ahukumiwe anakuwa na miaka mingapi au akutwe hana kosa analipwa fidia? Kama sio uonezi. Tunataka kuchambua kwa sababu nimesema kabisa amani ni tunda la haki, kama watu hawa hawatendewi haki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naapa hakutakuwepo na amani katika nchi hii mpaka tufike hapo, kwa sababu haki isipotendeka, amani natokea wapi wakati watu wanalalamika kila kona kwamba nimefanyiwa hivi, mimi unajua ilikuwa iwe hivi, nimefanyiwa hiki, kwa nini ifike mahali hapo, kwa nini tusione kwamba nchi ya amani haina migogoro, haina mambo ya kubambikiziwa, haina mambo ambayo ukiangalia kwa macho hata hivi unaona kabisa kwamba hii sio haki mtu kutendewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuongelea kuhusu watoto magerezani. Tunafahamu kabisa kwamba magereza yetu yanafanya kazi lakini Serikali ina mpango gani juu ya watoto wale walioko magerezani ambao wanazaliwa magerezani. Hivi kweli mtoto afungwe pamoja na mzazi wake kwa kosa ambalo hakufanya. Kwa nini isitokee kwamba mtu akishajifungua apewe kifungo cha nje ili yule mtoto aweze kupata haki za msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefika pale Ruanda nimekuta mtoto amefungwa na mzazi wake, akipita pale mlangoni kuingia na mtoto ananyoosha mikono hivi kuingia kama mfungwa, ametoka shule anaingia na yeye kama mfungwa, huyu mtoto anajifunza nini labda katika maisha yake atakuwa amejifunza nini? Serikali jamani tunaenda wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutasema kwamba kuna amani, huyu mtoto anayejifunza mambo mabaya ya gerezani atakapokuwa atakuwa mbaya kuliko baba yake au mama yake aliyeingia gerezani, kwa sababu atakuwa amejifunza ukatili. Kwa nini ifike mahali tumfunge mtoto yule ambaye hajafanya kosa? Kwa nini tusichukue hatua zingine za kum-rescue yule mtoto ili aje awe kijana mzuri au kijana bora katika maisha yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri anapo-windup atuambie hawa watoto watafungwa magerezani mpaka lini? Kwa sababu kama ni makosa walifanya wazazi wao na wakati mwingine mimba zenyewe zinapatikana humo humo magerezani, sasa yeye amekosa nini? Hajaingia jela yeye na wala mahakama haikumhusu yeye, kwa nini afungwe kama mfungwa wa kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuzungumzia kuhusu matumizi mabaya ya silaha au nguvu inayotumika na polisi katika kukamata mtu. Ifike mahali Serikali watueleze vizuri hivi anaponikamata mimi na begi langu kwa kunikwida na kunipiga na kunifanyaje wakati sina silaha, sina nguvu kama yeye ambaye amejifunza nguvu za kumkamata, mtu ni nini hiki kinatendeka jamani? Tunatambua amani huyu mtu anayefanyiwa haya ndani ya moyo wake anafurahi au ndugu zake wanaoona anatendewa hayo wanafurahi? Kama hawafurahi, hawana amani hawa watu, hawana furaha na Serikali yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini tufike hapo, kwa nini tusifike mahali pa kufanya yale tuliyokuwa tunafanya enzi zetu miaka hiyo. Serikali zilikuwa zinafanya mambo haya haya na watu hawa hawa tuliopo tumeshuhudia mengi, haya tunayoona ni mageni. Mtu anakuja anakamatwa au polisi wanatawanya maandamano au wanatawanya watu ambao wako mikusanyiko. Hii mikusanyiko haina silaha, haina chochote unaamua kutumia risasi ambazo tunazinunua kwa pesa nyingi kufyatua na kuumiza watu ambao ni nguvu kazi. Hivi tunaenda wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, ukiuliza hivi kwa nini mnafanya hivi? Eti kutoka juu, mbinguni? Yaani iwe ndio kinga tunataka kujua kutoka juu, huko juu kuna nini? Tunajua huko juu anakaa Mungu peke yake, Mheshimiwa Waziri atueleze huko juu kuna nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye ukamataji holela nimeshangaa kitu kimoja jamani. Sisi tulikuwepo hapa Bungeni siku moja tunashangaa watu wanakamatwa, Wabunge wanakamatwa wanaambiwa kwamba sijui wamempiga Shonza tulishangaa na ile immunity iko wapi?