Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwanza kwa Jeshi la Polisi kwa kazi nzuri wanayofanya. Pili, nampongeza Waziri Mheshimiwa Mwigulu Nchemba kwa kazi yake nzuri anayofanya. Pia namshukuru sana kwa kutupatia gari la Kituo cha Polisi Mtowisa, ahsante sana. Hata hivyo, palipo na mazuri hapakosi changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Kwela yapo mauaji ya mara kwa mara. Kwa mfano mwezi wa Pili Ndugu Paul Kisiwa, Mwenyekiti wa Kamati wa Chama cha Mapinduzi Kata ya Mtowisa ameuawa kinyama na watu wasiojulikana. Mwezi huu tarehe 2 Mei, 2018 Ndugu Benedict Chapewa, Mtendaji wa Kata ya Mwadui na aliyekuwa Katibu Mwenezi 2010 - 2015 ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaishauri Serikali kukomesha mauaji haya kwa kujenga Vituo vya Polisi kwa na kuvipatia bunduki. Jambo la kushauri ukanda ule wa bonde la Ziwa Rukwa kuwe na Wilaya ya Kipolisi hii ni kutokana na jiografia ilivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tunaomba Serikali kusaidia vituo ambavyo vimeanzishwa kujengwa na wananchi. Vituo cha Polisi vya Ilemba, Milepa na Kipeta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.