Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuwapongeza Waziri na Naibu wake kwa kazi nzuri kwa kazi wanazofanya. Wizara hii ina changamoto nyingi sana. Hata hivyo, nawapongeza Majeshi yetu yote ya Polisi, Magereza, Uhamiaji na Zimamoto. Kufuatia bajeti ya Wizara hii naomba kuwasilisha changamoto za Gereza Kuu la Kitai kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni uchakavu wa nyumba za watumishi. Hakuna uhaba wa nyumba za watumishi katika Gereza hilo, isipokuwa eneo la Gereza hilo lina tatizo la mchwa. Nyumba nyingi mapaa yake yameliwa na mchwa, hivyo zinavuja na hivyo zinaweza kuanguka wakati wowote na kuhatarisha maisha ya watumishi na familia za wanaoishi katika nyumba hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile kuna uchakavu wa jiko pamoja na mesi ya chakula. Paa nalo limeliwa na mchwa, mesi haina sakafu, wafungwa wanapikia nje kwani jiko limevunjika kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukosefu wa mlango wa Gereza; lango kuu la Gereza hilo ni chakavu sana kiasi kwamba inawapa ugumu sana wa ulinzi wa wafungwa. Lango hilo linahitaji ukarabati mkubwa sana. Uchakavu wa uzio (fence) iliyopo ni ya miti ambayo siyo imara, hivyo fence au uzio huo unahitaji kuangaliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nizungumzie kuhusu tatizo la maji safi na salama. Gereza lilifanikiwa kuchimba kisima. Kinachohitajika ni jenereta ama umeme jua ili kusukuma maji hayo kwa matumizi ya Gereza hilo. Tunaomba Mheshimiwa Waziri wa Nishati ili afanye hima kupeleka umeme katika Gereza hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni upungufu wa sare za Askari na wafungwa. Tunaomba sana Mheshimiwa Waziri alingalie hili, kwani wafungwa wamekosa uniform kiasi cha ku-repair sare hizo kwa mkono.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu ukosefu wa gari kwa ajili ya kazi za utawala. Gereza hili halina kabisa gari, jambo ambalo linaleta ugumu sana katika kutekeleza majukumu ya kiutawala. Naomba hili lipewe kipaumbele kwa namna yoyote ile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho, naomba Vituo vyetu vya Polisi vya Mbinga Wilayani; Kituo cha Polisi, Maguu na Kituo cha Litembo, vitengewe fedha kwa ajili ya ukarabati pamoja na kupatiwa vyombo vya usafiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha na naunga mkono hoja.