Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi Wilaya ya Igunga linafanya kazi nzuri katika kulinda raia, lakini Jeshi hilo lina changamoto nyingi sana zikiwemo ukosefu wa miundombinu kwa ajili ya kutenda kazi zao. Wilaya ya Igunga ina Kata 35, lakini ina vituo saba tu vya Polisi vya Igunga, Nanga, Simbo, Igurubi, Simbo, Sungwizi na Choma. Vituo hivi vyote vinatumia magari mawili tu yaliyopo kituo kikuu cha Wilaya Mjini Igunga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Polisi wetu wanafanya katika mazingira magumu sana. Kuna wakati wanalazimika kukodi pikipiki hata baisketi kwenda kukamata wahalifu. Hii ni aibu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Askari wetu wanaishi Mtaani na wengine wanaishi kwenye nyumba mbaya sana (Line Police). Hii haikubaliki. Naomba sana Serikali ijenge nyumba za Askari wetu kwani wanaishi kwa taabu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi, Igunga hakina jengo la utawala kwa ajili ya upelelezi. Tumeanza kujenga kwa kuchangishana na sasa tumefikia kupaua. Tunaomba Wizara ituunge mkono kwenye ujenzi huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Gereza la Wilaya ya Igunga ni dogo sana. Linahudumia wafungwa zaidi ya 200 badala ya wafungwa 100. Pia kuna Gereza kwa ajili ya akinamama. Kwa hiyo, tunalazimika kupeleka mahabusu na wafungwa Gereza la Nzega. Gereza hilo halina jengo la utawala, pia halina ngome. Ngome yake ni miti, aibu kubwa. Nilishawahi kumwomba Mheshimiwa Waziri atutembelee mara kadhaa lakini sijafanikiwa. Tafadhali Mheshimiwa Waziri aje Igunga ajionee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Viongozi wa Gereza la Igunga wakashirikiane na viongozi wa Wilaya wakiwemo Wabunge. Tumeanzisha ujenzi wa jengo la utawala ili kuondokana na aibu hii kwa kutumia fedha za Mfuko wa Jimbo na michango mingine. Tumekamilisha ujenzi wa msingi. Tunaomba Wizara ikamilishe jengo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, Askari Magereza nao hawana nyumba za makazi. Tunaomba wajengewe nyumba kwani wanateseka sana mitaani. Tafadhali tusaidieni Igunga Gereza letu lipo katika hali mbaya.