Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Polisi wanapostaafu hawapatiwi haki zao stahiki kwa wakati. Kwa mfano, waliostaafu mwaka 2017 mwishoni wanatakiwa wahame kwenye nyumba za Polisi kabla ya mwisho wa mwezi huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muundo wa Jeshi letu la Polisi kuwa chini ya Wakuu wa Mikoa na wa Wilaya (Kamati za Ulinzi na Usalama) linawaweka katika hali ngumu kiutendaji (Rejea Ibara ya 147 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania).

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi Himo kinafanya kazi kubwa (huduma eneo la mpakani na nchi jirani), hawana vitendea kazi vya kutosha hasa magari; Ofisi ni ndogo na ni chakavu; makazi yao hayatoshelezi na chakavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, weledi wa Jeshi letu la Polisi uwekwe msisitizo hasa mahusiano na jamii (elimu endelevu)