Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaendelea kuona mmomonyoko wa kasi wa kimaadili na wa ghafla wa Jeshi la Polisi na kushamiri kwa kasi vitendo vya uvunjivu wa haki za binadamu. Polisi waliokuwa kimbilio leo wanakimbiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano, Mwanza mtoto anafariki kisa mama yupo mahabusu na mtoto hawezi kupewa matibabu; Ndugu Saguta Heche amekamatwa, amefungwa pingu na anauawa; Polisi na bodaboda kana kwamba hawajui sheria, kama mtu hajataka kutii hiyo Sheria ya Usalama Barabarani si anafikishwa mahakamani; na upelelezi unaogusa Afisa wa Jeshi la Polisi haukamiliki au unachukua muda mrefu, liko wapi faili la Akwilina?

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu vyombo vya dola kugeuka wanasiasa, hii inafanyika makusudi kabisa. Tumezoea kuambiwa dola ina mkono mrefu lakini leo ndiyo tumeelewa maana halisi ya neno hilo. Dola ina mkono mrefu dhidi ya wenye mtazamo tofauti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano, kuendelea kukamata vijana wadogo wanaoandika tu kwenye mitandao, mbona hawamkamati Musiba? Je, ni kwa kuwa anaongea wanachotaka kukisikia? Mheshimiwa Tundu Lissu kisa kaandika tu meseji kwenye group wanamkamata, akina Mheshimiwa Zitto, Mheshimiwa Mbowe na wengine, ina maana hao Polisi hawajawahi kumsikia Musiba?