Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza Waziri, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu na Naibu Waziri Mheshimiwa Injinia Masauni kwa kazi nzuri wanazofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu utajikita katika maeneo matatu. Kwanza ni kuongeza askari Kituo cha Polisi Nanyamba. Kituo cha Polisi Nanyamba kilijengwa miaka mingi kuhudumia wakazi wa Nanyamba kama tarafa. Mwaka 2015 ilianzishwa Halmashauri ya Mji Nanyamba na Jimbo la Nanyamba. Kituo hicho sasa kimechakaa na idadi ya askari ni wachache. Naomba idadi ya askari iongezwe, kituo kipya kijengwe na wapewe na usafiri ili waweze kukabiliana na changamoto zinazojitokeza kwa kuwa kuna ongezeko kubwa la watu na uhalifu na wahalifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni ujenzi wa nyumba za askari. Kuna upungufu mkubwa wa nyumba za askari katika Mkoa wa Mtwara na katika Halmashauri ya Mji Nanyamba. Katika Halmashauri ya Mji Nanyamba hakuna nyumba ya askari na kuna kituo cha polisi. Naomba mgao wa nyumba mpya kwa Mkoa wa Mtwara na Jimbo la Nanyamba kwa ajili ya askari wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, ni changamoto za ulinzi na usalama kwa maeneo ya mpakani. Kuna changamoto ya usalama kwa maeneo tunayopakana na nchi jirani ya Msumbiji. Naomba askari wa Nanyamba wawezeshwe vitendea kazi ili waweze kufanya patrol maeneo ya Kifaya ambako kuna mwingiliano na wenzetu wa Msumbiji.