Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kuhusu hali ya amani nchini. Nashauri Serikali kuangalia upya juu ya suala zima la chanzo cha amani kama kipo vizuri. Chanzo cha amani ni haki. Haki ni tunda la amani, bila haki haitatokea hata siku moja amani ikawepo. Kamata kamata ambayo inaendelea hapa nchini na mauaji yanayoendelea yanachochea uvunjifu wa amani. Niishauri Serikali kuangalia kuna shida gani inayosababisha watu kuuliwa katika mazingira ya kutatanisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee juu ya polisi kubambikia kesi wananchi na kuwafanya kukaa mahabusu kwa miaka sita bila kesi zao kumalizwa mapema. Niishauri Serikali kuangalia juu ya mahabusu hawa kwani huongeza msongamano magerezani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali juu ya polisi kutumia nguvu nyingi kwenye mambo ya kawaida, mfano, unapozuia au kutawanya waandamanaji wasio na silaha kwa bunduki na risasi za moto mpaka kufikia kuua kama alivyouwa Ndugu Akwilina. Maandamano ya CHADEMA yalikuwa ya amani, hayakutakiwa kufyatuliwa risasi za moto. Polisi wameshindwa kufanya kazi ambayo wana wajibu nayo wanafanya kazi ya siasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee juu ya polisi wanavyowachukua watuhumiwa ndivyo sivyo, ni hatari sana kwani huwapiga watuhumiwa ambao hawajahukumiwa, hivyo kupewa hukumu na polisi kitu ambacho si haki. Je, kama haki haikutendeka, amani itatoka wapi? Hawa polisi wanaishi na wananchi huko kwenye jamii, hivyo itafika siku ambapo jamii itachoka na kupambana na polisi huko huko kwenye jamii.