Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali na Wizara kwa kuendeleza vyema kulinda usalama na raia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitabumbilisho vya Taifa (NIDA), zoezi la kuandikisha watu na kupata vitambulisho vya Taifa linaendelea katika mikoa mbalimbali nchini, lakini changamoto iliyopo ni uhaba wa fedha za kuendeshea zoezi mpaka inalazimu Madiwani, Wabunge na Watendaji wa Wilaya, Kata na Vijiji kuchanga pesa kusaidia chakula na malazi jambo ambalo linaweza kuathiri utendaji na mazingira hayo yanaweza weka ushawishi wa watendaji kutoa utambulisho kwa watu wasio na sifa yaani njia ya rushwa kutokana na malipo ya makarani kuwa madogo yaani shilingi elfu kumi kwa siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uendeshaji zoezi kwa kata ni ngumu kutokana na kata nyingine ni kubwa inaleta usumbufu kwa wazee, wagonjwa, mama wajawazito, hivyo zoezi liwe linazingatia umbali kati ya kijiji na kijiji ndani ya kata. Tunahitaji Waziri atoe tamko la namna bora ya kuendesha na pia upatikanaji wa vifaa na fedha ikiwemo magari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Madeni ya Askari Polisi katika TRC, jeshi la polisi hutumika na Shirika la Reli katika escort za treni na mkataba ni kuwa walipwe posho lakini kuna madai ya muda mrefu kati ya Askari na TRC mpaka kupelekea kufungua kesi Dodoma Mahakama Kuu. Naomba Serikali ifanye mazungumzo na TRC ili kuwe na malipo kwa wakati na madeni ya nyuma yalipwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi Nsimbo, Halmashauri ya Nsimbo Kituo cha Polisi ambacho bado hakina vifaa vya kutosha kuanzia gari, pikipiki na hifadhi ya silaha. Tunaomba Wizara isaidie vifaa hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria za barabarani, sheria zinazosimamiwa na Jeshi la Polisi juu ya makosa ya barabarani zinaingiliana na Wizara ya Ujenzi kupitia TANROAD hivyo ni vyema Serikali ikafanya sheria hizo ziwe chini ya Wizara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanuni za Sheria za Barabarani, wananchi wengi hawazijui kanuni hizi. Mfano makosa ya gari na dereva, makosa kati ya mmiliki na Dereva mwajiriwa. Sheria iboreshwe ili kosa la Dereva lisiwe la mmiliki.