Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Pongezi nyingi kwa Waziri na Naibu wake kwa hotuba nzuri na kwa kazi nzuri hasa ya kusuluhisha migogoro ya wakulima na wafugaji.
Kwanza naomba Wizara yako ifuatilie tozo wanayotozwa wavuvi wa Mtwara, shilingi mia tano arobaini na saba kwa kilo ya samaki. Je, ni tozo ya watu binafsi? Kimsingi tozo hii imeathiri uchumi wa wavuvi wa Mtwara na naomba Mheshimiwa Waziri atembelee Mkoa wa Mtwara kama alivyofanya kwa jamii za wakulima na wafugaji.
Pili, napongeza jinsi Wizara ilivyoongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji katika nchi yetu. Umwagiliaji huu kwa kiasi kikubwa ni kwa mazao ya chakula cha wanga. Ushauri wangu kwa Wizara ni kuongeza uzalishaji wa mbogamboga na matunda kwa kuwezesha umwagiliaji wa matone (Drip Irrigation).
Hoja yangu inatokana na hali halisi ya upatikanaji wa mboga na matunda kwa msimu fulani ambapo wakati mwingine bidhaa hizi huadimika na kupelekea bei kupanda kwa kiasi kikubwa. Athari za hali hii zinaweza kuonekana katika lishe ya jamii kuwa duni. Hivyo, naomba wataalam wa Wizara wajitahidi kuwaandaa wananchi pale watakapopata mikopo ya milioni hamsini wengine wawekeze kwenye kilimo cha mbogamboga na matunda kwa (Drip irrigation).
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. „Kama mnataka mali mtaipata shambani‟