Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, upandishaji vyeo Jeshi la Zimamoto; Askari walipandishwa vyeo baada ya mafunzo mwaka 2016 na walipewa barua za kupanda vyeo, lakini hawajabadilishiwa mshahara mpaka leo na badala yake kuna barua ya kufuta vyeo vilivyopanda. Naomba kujua lini Askari hawa watarejeshewa vyeo na mabadiliko ya mishahara yao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ya Kituo cha Polisi Kati Geita; katika bajeti ya mwaka 2016/2017, Serikali iliahidi ujenzi wa kituo hiki. Naomba kufahamu lini ujenzi huu wa kituo cha Polisi Kati Geita Mjini utaanza, ikiwa ni pamoja na jengo la zimamoto na magari?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uhaba wa magari, lipo tatizo kubwa la usafiri kwa Jeshi la Polisi Mkoani Geita. Mfano OCD Geita anategemea gari la FFU Kasamwa inapotokea ugeni wa viongozi hali za doria zimepungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mlundikano wa mahabusu na ubovu wa Magereza; hali katika Gereza la Geita ni mbaya sana, idadi ya mahabusu ni wengi na hii imetokana na utaratibu mbaya wa kesi za kawaida ambazo zingeweza kumalizwa na wahusika, kulazimu kupelekwa Polisi na Mahakamani ambapo matokeo yake mahabusu mwenye kesi ya kuku kutumia gharama kubwa bdala ya faida inakuwa hasara. Naishauri Serikali kuleta mfumo utakaoondoa watu kujazana mahabusu na magereza kwa sababu hili linasababisha mateso na rushwa.